Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 8:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Hivi ndivyo munavyopaswa kufanya: Kila mumoja wenu amwambie mwenzake ukweli. Tribinali zenu zitoe siku zote hukumu za haki zinazoleta amani.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 8:16
29 Referans Kwoze  

Kwa hivi, muache uongo! Kila mumoja aseme ukweli kwa mwenzake, kwa maana sisi wote ni viungo vya mwili mumoja.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Mutoe hukumu kwa haki, mutende mema na kuwa na huruma ninyi kwa ninyi.


Ni mutu anayefanya hivi: anaishi katika ukamilifu, anatenda kwa haki siku zote, anasema ukweli kutoka ndani ya moyo, hatetani, hatendei rafiki yake uovu, hamutukani jirani yake, anazarau wapotevu, anaheshimu wanaomwabudu Yawe, hageuzi kiapo chake hata kikimuletea hasara, hakopeshi feza yake kwa kupata faida, wala kupokea kituliro kumutesa asiyekuwa na kosa. Mutu anayefanya vile, hatatikisika hata kidogo.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Ukweli unadumu milele, lakini uongo ni wa muda kidogo tu.


Musema kweli anatoa ushuhuda wa kweli, lakini mushuhuda wa uongo anasema udanganyifu.


Lakini watu wenye woga, wasioamini, wenye machukizo, wauaji, wazinzi, wachawi, wanaoabudu sanamu na wote wanaosema uongo, fungu lao ni katika lile ziwa la moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto. Hiki ndicho kifo cha pili.”


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


Basi, kwa jina la Bwana ninawaonya hivi: musiishi tena kama watu wa mataifa mengine, wanaofuata mawazo yao ya bure


Heri wale wanaoleta amani, maana wataitwa watoto wa Mungu!


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Lakini muache haki itiririke kama maji, usawa ukuwe kama muto usiokauka.


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Musiibe, musidanganye wala kuambiana uongo.


Yawe anasema hivi: Mufuate sheria yangu na kutenda kwa haki. Muokoe kila mutu aliyenyanganywa mali zake toka katika mikono ya mutesaji. Musiwatendee vibaya au kwa ukali wageni, wayatima na wajane, wala musimwange damu ya mutu asiyekuwa na kosa kwa nafasi hii.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninyi wakubwa wa Waisraeli, mumefanya zambi vyakutosha. Muache kutesa watu kwa ukali. Muimarishe sheria yangu na haki. Muache kuwafukuza watu wangu katika inchi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Ujiepushe na uovu, utende mazuri; utafute amani na kuifuatilia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite