Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 8:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 8:12
39 Referans Kwoze  

Juu ya kabila la Yosefu akasema: “Yawe abariki inchi yake, kwa baraka nzuri kabisa kutoka juu,


Mungu akumiminie umande wa mbinguni, akupe udongo wenye mboleo, ngano na divai kwa wingi.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa watu hawa waliobaki, hali hii inaonekana kuwa kitu kisichowezekana; lakini munazani haiwezekani kwangu mimi? –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.


Ingawa sasa hakuna ngano ndani ya gala, nayo mizabibu, tini, mikomamanga na mizeituni haijazaa kitu, lakini tangu leo, nitawabariki.


Ndiyo maana mbingu zimeacha kunyesha mvua, nao udongo hauoteshi mavuno.


Musiogope, enyi nyama, malisho katika mbuga yamekuwa mazuri, miti inazaa matunda yake, mizabibu na mitini zinazaa kwa wingi.


Na tunda la haki linapandwa katika amani na wale wanaopenda amani.


Basi mutu asijivune kwa ajili ya wanadamu. Kwa maana vitu vyote ni vyenu:


Yawe anasema: Nitaponyesha ukosefu wao wa uaminifu; nitawapenda tena kwa moyo wangu wote, maana sitawakasirikia tena.


Nitayazidisha matunda ya miti na mazao ya mashamba kusudi musizarauliwe tena kwa ajili ya njaa kati ya mataifa.


Kwa vile mulipata haya mara mbili, watu wakaona kwamba mazarau ni majaliwa yenu, sasa mutapata sehemu mara mbili kuwa mali yenu, na furaha yenu itadumu milele.


Mutakapopanda mbegu zenu, Yawe atanyesha mvua kwa wakati wake, nazo zitakomaa na kuwapa mavuno mengi mazuri. Makundi yenu ya nyama nao watakula katika mashamba makubwa ya kukulishia nyama.


Mwaka ule Isaka akapanda mbegu katika inchi ile, akavuna mara mia zaidi, maana Yawe alimubariki,


Nitawafanya watu wangu Waisraeli watembee juu yenu. Nanyi mutakuwa urizi wao, wala hamutawafanya tena wakufiwe na watoto wao.


Kasirani ya mufalme ni kama ngurumo ya simba, lakini upendo wake ni kama umande juu ya majani.


Milima ilete ustawi kwa watu wako, vilima vijae haki.


Kwa hiyo, watu wa Israeli wakakaa salama, wazao wa Yakobo peke yao, katika inchi iliyojaa ngano na divai, inchi ambayo anga lake linadondosha umande.


Mafundisho yangu yatone kama mvua, maneno yangu yadondoke kama umande, kama manyunyu kwenye mimea michanga, kama mvua nyepesi katika majani mabichi.


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Kama mukifuata masharti yangu na kushika amri zangu,


Uaminifu utachipuka katika inchi; haki utashuka toka mbinguni.


Basi, watatoweka kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi; kama makapi yanayopeperushwa kwenye nafasi ya kupepetea, kama moshi unaotoka katika munara wa kutoshea moshi inje.


Sasa, mufikiri vizuri juu ya mambo yatakayotukia. Leo ni siku makumi mbili na ine ya mwezi wa kenda, siku ambayo musingi wa hekalu umekamilika. Basi mufikiri vizuri:


Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.


Hawatakamatwa tena mateka na mataifa mengine wala nyama wa pori hawatawaua na kuwakula. Wataishi kwa usalama na hakuna atakayewatisha.


Mimi niko upande wenu, nitahakikisha kuwa udongo wenu utalimwa na kupandwa mbegu.


Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.


Waisraeli watakaobaki hawatatenda mabaya wala hawatasema uongo, wala kwao hakutapatikana mudanganyifu yeyote. Watapata chakula na kulala wala hakuna mutu atakayewaogopesha.


Wadudu waharibifu nitawazuia wasiyaharibu tena mazao yenu. Mizabibu yenu katika mashamba haitaacha kuzaa matunda.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite