Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Munapokula na kunywa, si munakula na kunywa kwa ajili yenu wenyewe?

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 7:6
15 Referans Kwoze  

Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Kila kitu munachofanya au kusema, mufanye yote kwa jina la Bwana Yesu, kwa kumushukuru Mungu Baba kwa njia yake.


Hawatamutolea Yawe sadaka ya divai, wala hawatamufurahisha kwa sadaka zao. Chakula chao kitakuwa kama cha kilio, wote watakaokikula watajichafua. Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu, hakitafaa kuletwa katika nyumba kwa Yawe.


Basi siku ile wakakula na kunywa kwa furaha kubwa mbele ya Yawe. Kwa mara ya pili wakamuweka Solomono mwana wa Daudi kuwa mufalme. Wakamupakaa mafuta apate kuwa mutawala katika jina la Yawe, na Zadoki akuwe kuhani.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


muzitumie hizo feza kwa kitu chochote mutakachopenda - nyama ya ngombe, nyama ya kondoo, divai au kinywaji kikali. Mutavikula na kufurahi hapo mbele ya Yawe, Mungu wenu, pamoja na jamaa zenu.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


Hamujaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa sadaka zenu. Nami sikuwalemea ninyi kwa kutaka sadaka, wala sikuwachokesha kwa kuwadai ubani.


Ninyi munaniuliza: Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni? Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali? Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula, munatafuta tu furaha yenu wenyewe na kuwagandamiza watumishi wenu!


Uwaambie wakaaji wote wa inchi na makuhani hivi: Kwa muda wa miaka makumi saba iliyopita, ninyi mulikuwa mukifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba. Munazani mulifunga kwa ajili yangu?


Haya ndiyo mambo ambayo mimi Yawe niliyowaambia kupitia kwa manabii wa zamani, wakati Yerusalema ulikuwa umestawi na wenye wakaaji tele, na wakati ambapo kulikuwa wakaaji wengi katika miji ya kandokando yake na katika eneo la Negebu na mabonde ya Sefela.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite