Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 7:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Uwaambie wakaaji wote wa inchi na makuhani hivi: Kwa muda wa miaka makumi saba iliyopita, ninyi mulikuwa mukifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba. Munazani mulifunga kwa ajili yangu?

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 7:5
27 Referans Kwoze  

Halafu yule malaika wa Yawe akasema: Ee Yawe wa majeshi, kwa muda gani utaendelea kutokuwa na huruma juu ya muji Yerusalema na miji ya inchi ya Yuda ambayo umeikasirikia kwa muda wa miaka makumi saba?


Basi, kama mukikula au mukikunywa, au mukifanya neno lolote, mufanye yote kwa ajili ya utukufu wa Mungu.


Munapokula na kunywa, si munakula na kunywa kwa ajili yenu wenyewe?


na kuwauliza makuhani wa hekalu la Yawe wa majeshi maneno haya: Tuendelee kuomboleza na kufunga kula chakula katika mwezi wa tano kama tulivyofanya kwa muda wa miaka mingi sasa?


Na kila kitu munachofanya, mukifanye kwa moyo wenu wote, kama vile wenye kumutumikia Bwana wala si watu.


Naye alikufa kwa ajili ya watu wote, kusudi wale wanaoishi, wasiishi kwa ajili yao wenyewe, lakini kwa ajili ya yule aliyekufa na kufufuka kwa ajili yao.


Wanafanya matendo yao yote tu kusudi wajionyeshe mbele ya watu. Wanajifungia kwa paji za nyuso vibweta vipana vyenye vikaratasi vya Maandiko Matakatifu. Nao wanavaa kanzu zenye pembe ndefu.


“Munapofunga kula chakula, musifanye kama wanafiki, wanaojigeuza kuwa wenye sikitiko na kukunja nyuso zao, kusudi watu waone kwamba wanafunga. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


“Basi wakati unapomusaidia masikini, usipige baragumu, kama vile wanafiki wanavyofanya katika nyumba za kuabudia na katika barabara kusudi wasifiwe na watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Siku za mafungo ya kula chakula ya mwezi wa ine, mwezi wa tano, mwezi wa saba na mwezi wa kumi, zitakuwa nyakati za furaha na shangwe; zitakuwa sikukuu za shangwe kwa watu wa Yuda. Basi, mupende ukweli na amani.


Inchi hii yote itakuwa katika mabomoko matupu na ukiwa, na mataifa jirani yatamutumikia mufalme wa Babeli kwa muda wa miaka makumi saba.


Kisha wakubwa wote wa waaskari pamoja na watu wao waliposikia kwamba mufalme wa Babeli alimuchagua Gedalia kuwa mutawala, wakamwendea Gedalia kule Mispa. Watu hao walikuwa ni: Isimaeli mwana wa Netania, Yohana mwana wa Karea, Seraya mwana wa Taumeti wa muji wa Netofati, na Yazania mwana wa Mumakati.


Hamujaniletea kondoo wenu wa sadaka za kuteketezwa, wala kuniheshimu kwa sadaka zenu. Nami sikuwalemea ninyi kwa kutaka sadaka, wala sikuwachokesha kwa kuwadai ubani.


Ninyi munaniuliza: Kwa nini tunafunga kula lakini wewe hauoni? Mbona tunajitesa, lakini wewe haujali? Ukweli ni kwamba wakati munapofunga kula, munatafuta tu furaha yenu wenyewe na kuwagandamiza watumishi wenu!


Yawe anasema hivi: Mutakapopitisha miaka makumi saba huko Babeli, nitawashugulikia na kuitimiza ahadi yangu ya kuwarudisha kwa nafasi hii.


Katika siku ya kumi ya mwezi wa tano, mwaka wa kumi na kenda wa utawala wa Nebukadneza, mufalme wa Babeli, Nebuzaradani mukubwa wa waaskari wa mufalme ambaye alimutumikia mufalme wa Babeli, aliingia Yerusalema.


mimi Danieli nilikuwa nikisoma kwa uangalifu vitabu vitakatifu, na humo nikaelewa maana ya jambo lile Yawe alilomufahamisha nabii Yeremia juu ya ile miaka makumi saba, muda ambao utahusika na kuharibiwa kwa Yerusalema.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Halafu, neno la Yawe wa majeshi lilinifikia kusema hivi:


Katika mwezi wa saba, Isimaeli mwana wa Netania, mujukuu wa Elisama, aliyekuwa wa ukoo wa kifalme, akafika kwa Gedalia pamoja na watu kumi, akamushambulia Gedalia, akamwua. Vilevile, akawaua Wayuda na Wababeli waliokuwa naye.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite