Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Nami niliwatawanya kwa upepo mukali kati ya mataifa yote ambayo hawakuyajua. Hivyo inchi waliyoiacha ikabaki tupu; hapakuwa mutu yeyote aliyekaa mule; inchi hiyo ya kupendeza ikakuwa ukiwa.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 7:14
35 Referans Kwoze  

Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.


“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,


Angalia, zoruba kali kutoka kwa Yawe; kasirani yake imeamuka, upepo mukali utapiga kichwa cha mwovu.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


Basi, nikamwuliza: Unakwenda wapi? Naye akanijibu: Ninakwenda kuupima urefu na upana wa Yerusalema.


Yawe anasema: Nimeyateketeza kabisa mataifa; kuta zao za kujikinga ni mabomoko. Barabara zao nimeziharibu, na hakuna anayepita ndani yake. Miji yao imekuwa mitupu, bila watu, na bila wakaaji.


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


Umetoboa vichwa vya wakubwa wao kwa mikuki yao wenyewe, waliotufikia kama zoruba kututawanya, wakijivuna kwa kuwameza wamasikini kwa siri.


Yawe hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu, Yawe hatawaachilia wenye makosa hata kidogo. Yawe anapopita, upepo mukali na zoruba vinatokea; mawingu ni mavumbi yanayonyanyuliwa na miguu yake.


Basi, nitashusha moto juu ya kuta za muji wa Raba, na kuziteketeza kabisa nyumba zake nzuri. Siku hiyo ya vita kutakuwa makelele mengi, nayo mapambano yatakuwa makali kama zoruba.


Na tokea ndani ya moja ya pembe hizo ine, kuliota pembe ingine dogo, ikakomaa sana kuelekea upande wa kusini-mashariki, na kuelekea inchi ile nzuri sana.


Mwaka wa makumi mbili na tatu wa utawala wa Nebukadneza, Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme, aliwapeleka Wayuda mia saba na makumi ine na watano. Jumla ya watu wote ilikuwa watu elfu ine mia sita.


Kwa hiyo, kasirani yangu na hasira yangu iliwaka na kumwangika juu ya miji ya Yuda na barabara za Yerusalema, hata kukakuwa jangwa na mabomoko kama inavyokuwa mpaka leo.


Kisha wakubwa hao wakamwambia Baruku: Wewe uende ujifiche pamoja na Yeremia, na kusikuwe mutu yeyote atakayejua pahali munapokuwa.


Angalia, zoruba kali kutoka kwa Yawe! Kasirani yake imeamuka, upepo mukali utapiga kichwa cha mwovu.


Na kwa ngambo yenu ninyi watu wa Israeli, ninaleta taifa moja kutoka mbali kuwashambulia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Hili taifa haliwezi kushindwa, ni taifa la zamani, ni taifa ambalo hamufahamu luga yake. Hamuwezi kuelewa hata neno wanalolisema.


Ujumbe wa Mungu juu ya jangwa kando ya bahari. Kama upepo mukali unaovuma kutoka kusini, washambulizi wanakuja kutokea katika jangwa, kutoka katika inchi ya kutisha.


Mataifa yananguruma kama ngurumo ya maji mengi, lakini Mungu atayakaripia, nayo yatakimbilia mbali. Yatafukuzwa kama maganda juu ya mulima mbele ya upepo; kama mavumbi yanayonyanyuliwa na upepo mukali.


watoweke kama konokono anavyoyeyuka akitembea, kama mimba iliyoharibika isiyoona jua hata kidogo!


Na hivyo likatimia neno la Yawe alilosema kwa njia ya nabii Yeremia: “Mpaka inchi imetimiza Sabato zake, haitalimwa siku zote itakapokuwa ukiwa mpaka miaka makumi saba itakapotimia.”


“Yawe ataleta kutoka mbali taifa moja liwashambulie mbio kama tai, taifa ambalo hamujui luga yake.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


Nitaleta nyama wakali kati yenu ambao watawanyanganya watoto wenu na kula mifugo yenu na kupunguza hesabu yenu hata njia zenu zigeuke kama jangwa.


Yawe atakuja kama moto, na magari yake ya vita ni kama zoruba. Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali, na maonyo yake yatimizwe kwa ndimi za moto.


Wewe ulikuwa umeachwa na kuchukiwa, hakuna aliyependa hata kupita ndani yako. Lakini sasa nitakufanya ukuwe na utukufu milele, utakuwa muji wa furaha kwa kizazi na kizazi.


Wachungaji wengi wameharibu shamba langu la mizabibu, wamekanyagakanyaga chini urizi wangu; shamba langu zuri wamelifanya jangwa.


Hukohuko katika muji wazazi watawakula watoto wao wenyewe na watoto watawakula wazazi wao. Nitatimiza hukumu zangu juu yenu na watakaobaki wazima nitawasambaza pande zote.


Uwaambie watu wa inchi hii: Bwana wetu Yawe anasema hivi juu ya wakaaji wa Yerusalema ambao wangali bado katika inchi ya Waisraeli: Watakula chakula chao kwa hofu na kunywa maji yao kwa kufazaika, maana inchi yao haitakuwa na kitu, kwa sababu kila mukaaji ni mutesaji mukali.


Nitakusambaza kati ya mataifa na kukutupatupa katika inchi zingine. Nitaukomesha uchafu unaokuwa ndani yako.


Kama vile moto unavyoteketeza, Jeshi hilo linaharibu kila kitu mbele yake na kuacha nyuma kila kitu kinateketezwa; mbele ya kupita kwao, inchi ni kama bustani ya Edeni, lakini wakisha kupita, ni jangwa tupu. Hakuna kinachoweza kuponyoka!


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi: Yawe wa majeshi anasema hivi:


Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite