Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Wakaifanya mioyo yao kuwa migumu kama jiwe, wasipate kusikia sheria yangu mimi Yawe wa majeshi niliyoitangaza kwa roho yangu kwa kupitia manabii waliotangulia. Kwa hiyo, mimi Yawe wa majeshi nikawaka hasira juu yao,

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 7:12
34 Referans Kwoze  

Nitawapa moyo mupya na kuweka roho mupya ndani yenu. Nitauondoa ule moyo mugumu kama jiwe na kuwapa moyo musikilivu,


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka kuwa migumu, wameziba masikio yao na wamefunga macho yao. Isingekuwa hivi, wangeona na macho yao, wangesikia na masikio yao, wangefahamu na mioyo yao, na wangegeukia kwangu na ningewaponyesha.


Nitawapa moyo mupya na kuweka roho mupya ndani yenu. Nitauondoa kwenu moyo mugumu kama jiwe na kuwapa moyo musikilivu.


Wewe unachukia maonyo, na maneno yangu haupendi kuyafuata.


kusudi ‘Wapate kuangalia, lakini wasione; nao wapate kusikia, lakini wasikuwe na ufahamu, kusudi wasipate kumugeukia Mungu na kusamehewa.’ ”


Maana mioyo ya watu hawa imegeuka migumu, wameziba masikio yao, nao wamefunga macho yao, kusudi wasipate kuona, nao wasipate kusikia, wala wasipate kunigeukia, nami ningewaponyesha.’


Watu hao ni wenye kichwa nguvu na moyo mugumu. Ninakutuma kwao, nawe utawaambia: “Bwana wetu Yawe anasema hivi.”


Kisha akaniambia: Ufanye akili za watu hawa kuwa ngumu, masikio yao yasisikie, macho yao yasione; wasipate kuona kwa macho yao, wasipate kusikia kwa masikio yao, wasipate kuelewa kwa akili zao, na kunigeukia, nao wapate kupona.


Maana hakuna hata ujumbe wowote uliotetewa kwa mapenzi ya kimutu, lakini watu walipasha ujumbe wa Mungu wakiongozwa na Roho Mutakatifu.


Nafasi ile mbegu zilipoanguka pembeni ya njia ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu. Lakini Shetani anakuja na kuondoa lile neno katika mioyo yao kusudi wasiamini na kuokolewa.


Haya ndiyo mambo ambayo mimi Yawe niliyowaambia kupitia kwa manabii wa zamani, wakati Yerusalema ulikuwa umestawi na wenye wakaaji tele, na wakati ambapo kulikuwa wakaaji wengi katika miji ya kandokando yake na katika eneo la Negebu na mabonde ya Sefela.


Hezekia, mufalme wa Yuda, na watu wote wa Yuda hawakumwua Mika. Hezekia alimwogopa Yawe na kuomba rehema kwake. Naye Yawe akabadilisha nia yake ya kuleta hasara aliyokusudia juu yao. Lakini sisi tuko mbio kwa kujiletea hasara wenyewe.


Zambi ya watu wa Yuda, haiwezi kufutikana, imeandikwa kwa kalamu ya chuma; kwa chongo ya almasi. Imechorwa ndani ya mioyo yao na kwenye pembe za mazabahu yao.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Lakini nilikujua wewe kuwa na moyo mugumu; kichwa kigumu kama chuma, uso wako kama shaba.


Yeye ni mwenye hekima sana na nguvu nyingi. Nani aliyepingana naye, akashinda?


Sedekia alimwasi vilevile mufalme Nebukadneza aliyekuwa amemufanya aape kwa jina la Mungu kwamba hatamwasi. Alikuwa mupotovu sana na kufanya moyo mugumu, akakataa kumugeukia Yawe, Mungu wa Israeli.


Musikilize, enyi wenye vichwa vigumu, munisikilize enyi munaokuwa mbali na ukombozi.


Mimi Yawe nitaigusa mioyo ya Waisraeli kusudi wanirudilie, maana wamejitenga mbali nami kwa kuabudu sanamu zao za miungu.


Hata hivyo, moyo wa mufalme ulibaki tu kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza. Ikakuwa kama vile Yawe alivyosema.


Nimewapangia kifo kwa upanga, ninyi wote mutanaswa kwa kuchinjwa! Maana, nilipowaita, hamukuniitikia; niliposema, hamukunisikiliza. Mulitenda maovu mbele yangu, mukachagua yale nisiyoyapenda.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaimwanga hasira yangu juu ya pahali hapa, juu ya wanadamu na nyama, miti katika mashamba na juu ya mazao ya inchi. Nayo nafasi hii itawaka moto wala hautaweza kuzimishwa.


Ingawa hivyo babu zenu hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini walifanya vichwa vyao kuwa vigumu, wakakataa kusikia na kufuata maagizo yangu.


Leo mimi nimewaambia, lakini hamukutii neno lolote ambalo Yawe, Mungu wenu amenituma niwaambie.


Yawe alichukizwa sana na babu zenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite