Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 7:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Musiwatese wajane, wayatima, wageni au wamasikini; musipange kutendeana mabaya ndani ya mioyo yenu.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 7:10
38 Referans Kwoze  

wamenenepa na kungaa vizuri. Maovu yao hayana mwisho, hawahukumu yatima kwa kufuatana na sheria kusudi wapate kufanikiwa, wala hawatetei haki za watu wakosefu.


Kila mutu anayemuchukia ndugu yake ni mwuaji, nanyi munajua kwamba mwuaji yeyote hana uzima wa milele ndani yake.


Ninyi hamukulipa mishahara ya watumishi waliotumika katika mashamba yenu. Musikilize mashitaki yao! Malalamiko ya wavunaji yamefika katika masikio ya Bwana Mwenye Uwezo!


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Mufalme awatetee wamasikini wa taifa, awasaidie wakosefu, na kuwaangamiza watesaji.


Utawaangamiza wazao wao watoweke katika dunia; watoto wao hawatabaki kati ya wanadamu.


wizi, wenye tamaa, walevi, watukanaji, wanyanganyi, watu wale wote hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Mutu yeyote asikusudie kumutendea mwenzake ubaya wala musiape uongo, maana ninayachukia sana matendo hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Musikilize neno hili, enyi wanawake munaokuwa kama ngombe wa Basani munaokuwa kule juu ya mulima wa Samaria. Ninyi munaowaonea wamasikini, munaowagandamiza wakosefu, na kuwaambia waume zenu: Mutuletee divai tukunywe! Musikilize ujumbe huu:


Kila fasi katika inchi watu wanatendeana vibaya na kunyanganya kwa kinguvu. Wanagandamiza wamasikini na wakosefu, na kuwaonea wageni bila kujali.


Huko kwako kuna watu ambao wanapokea kitulizo kwa kumwanga damu. Wanakopesha kwa kudai faida ya juu, wananyanganya mali za wenzao kwa nguvu, na kunisahau mimi kabisa! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Kwako baba na mama wanazarauliwa. Mugeni anayekaa kwako ananyanganywa mali yake. Wayatima na wajane wanaonewa.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


moyo unaopanga mipango miovu, miguu inayokuwa mbio kutenda maovu,


Usipange maovu juu ya jirani yako anayeishi karibu nawe bila wasiwasi.


Ee Yawe, uniokoe na watu wabaya, unikinge na watesaji wakali.


“ ‘Alaaniwe mutu yeyote anayepotosha haki ya mugeni au yatima au mujane’. Na watu wote wataitika: ‘Amina!’


Usimutese mugeni. Ninyi munajua hali ya kuwa mugeni, maana mulikuwa wageni katika inchi ya Misri.


Kila anachosema ni uovu na uongo; ameacha kutumia hekima na kutenda mema.


Musiwatese wageni, wayatima au wajane au kuwaua watu wasiokuwa na kosa katika inchi hii. Musijiangamize wenyewe kwa kuabudu miungu mingine.


Enyi jamaa ya Daudi, Yawe anasema hivi: Kila asubui muamue maneno kufuatana na sheria yangu, muwakomboe wote walionyanganywa mali zao toka katika mikono ya watesaji. Kama si vile, hasira yangu itawaka kama moto, wala hakuna atakayeweza kuizimisha, kwa sababu ya matendo yenu maovu.


Muniachie watoto wenu wayatima nami nitawatunza; muwaache wajane wenu wanitegemee.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite