Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 6:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kisha yule malaika aliyeongea nami akaniambia kwa sauti: Wale farasi waliokwenda katika inchi ya kaskazini wameituliza kasirani ya Yawe.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 6:8
15 Referans Kwoze  

Ndivyo nitakavyomaliza hasira yangu, nami nitakuwa nimetuliza kasirani yangu na kufarijika ndani ya moyo. Hapo ndipo watakapojua kwamba mimi, Yawe, nimewaazibu kwa sababu ya wivu wangu kwa ukosefu wenu wa uaminifu.


Lakini nimekasirikia sana mataifa ambayo yanastarehe. Nilikuwa ninayakasirikia kidogo, lakini yaliwaongezea hasara.


Ewe Yerusalema, matendo yako machafu yamekuchafua. Ingawa nilijaribu kukutakasa, mwenyewe ulibaki muchafu. Basi, hautatakasika tena mpaka nitakapotuliza hasira yangu juu yako.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Hivi, kasirani yangu itatosheka juu yako, wivu niliokuwa nao juu yako utakwisha; nitatulia wala sitaona hasira tena.


Mukusanyike wote musikilize! Nani kati yenu alitabiri vitu hivi? Yule ambaye Yawe anamupenda atatimiza mapenzi yake juu ya Babeli, atawashambulia Wakaldea.


Kwa hiyo, nitawamwangia waadui zangu hasira yangu, nitawalipiza kisasi wapinzani wangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi, Mwenye Nguvu wa Israeli.–


Mutawala akikukasirikia, usiache kazi; makosa makubwa yanaweza kufutwa ukiwa munyenyekevu.


Samusoni akawaambia hao Wafilistini: “Kama hayo ndiyo muliyofanya, ninaapa kwamba sitaondoka mpaka nimelipiza kisasi.”


Mungu amewatia katika mikono yenu wale wakubwa wa Midiani, Kibombobombo na Imbwa-wa-Pori. Basi, mimi nimefanya nini nikilinganishwa nanyi?” Gideoni alipokwisha kusema hivyo, hasira yao juu yake ikatulia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite