Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Malaika akanijibu: Magari haya ni upepo kutoka pande ine za mbingu. Yalikuwa mbele ya Yawe wa dunia nzima, na sasa yanaondoka.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 6:5
29 Referans Kwoze  

Kisha mambo yale, nikaona wamalaika wane wakisimama kwenye pembe ine za dunia, wakizuiza upepo toka pande ine za dunia, kusudi usivume juu ya dunia, wala juu ya bahari, wala juu ya muti wowote.


Malaika ni nini, basi? Wao wote ni roho wanaomutumikia Mungu na wanaotumwa naye kwa ajili ya faida ya wale wanaopaswa kuokolewa.


Lakini juu ya wamalaika, Mungu alisema: “Mungu anawafanya wamalaika wake kuwa kama upepo. Anawafanya hao watumishi wake kuwa kama ndimi za moto.”


Halafu, Yawe akaniambia: Ewe mwanadamu, kwa ajili yangu toa unabii kwa upepo, uuambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ewe upepo kuja toka pande zote ine na kuipulizia miili hii iliyokufa kusudi ipate kuishi.


Baragumu kubwa itapigwa, halafu atawatuma wamalaika wake katika pande ine za dunia, kusudi wawakusanye watu wake aliowachagua, kutoka katika dunia nzima.


Halafu akaniambia: Hawa ndio wale watu wawili ambao Bwana wa ulimwengu wote aliwachagua kwa kuwapakaa mafuta kusudi wamutumikie.


Kutoka kiti hicho kijito cha moto kilibubujika, kikatiririka. Maelfu ya watu walimutumikia, na mamilioni walisimama mbele yake. Halafu waamuzi wakajitayarisha kwa kuhukumu, na vitabu vikafunguliwa.


Mimi Danieli niliona maono usiku. Ilikuwa hivi: Upepo ulivuma juu ya bahari kubwa toka pande zote ine za mbinguni.


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


mbona unauonea kijicho mulima Mungu aliouchagua akae juu yake? Yawe atakaa huko milele!


Basi, ikatukia siku moja wamalaika wa Mungu walikwenda kukutana mbele ya Yawe. Shetani akakuja kuwa pamoja nao.


Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.


“Mufanye angalisho, musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa sababu ninawaambia kwamba wamalaika wao wanaokuwa mbinguni wako siku zote karibu na Baba yangu anayekuwa mbinguni. [


Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.


Halafu wale makerubi waliyakunjua mabawa yao na kuanza kuruka pamoja na yale magurudumu yaliyokuwa pembeni yao, nao utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.


Mumusifu, enyi moto, mvua ya mawe na teluji, upepo wenye zoruba unaotimiza amri yake!


Yawe akamwambia: “Kwenda usimame juu ya mulima, mbele yangu mimi Yawe.” Basi, Yawe akapita na kuuvumisha upepo mukali ambao uliporomosha milima na kuvunja mawe makubwa. Lakini Yawe hakukuwa katika upepo ule. Upepo ukapita, kukakuwa tetemeko la inchi. Lakini Yawe hakukuwa katika tetemeko la inchi.


Muangalie, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote liko karibu kupita mbele yenu kuelekea muto Yordani.


Nitaleta upepo kutoka pande zote za mbingu; nitawatawanya kila pahali, wala hakutakuwa taifa lolote ambalo halitakuwa na wakimbizi wa Elamu.


Hata hivyo, wakati atakapokuwa na nguvu, ufalme wake utavunjika na kugawanyika katika sehemu ine kuelekea pande ine za mbingu. Wazao wake hawatatawala, wala ufalme hautakuwa katika mikono ya urizi aliotawala, kwa sababu ufalme wake utakamatwa na wengine.


Niliona maono mengine tena. Niliona magari mane ya vita yakitoka katikati ya milima miwili ya shaba nyeusi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite