Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 6:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Utatwaa feza na zahabu hiyo, utengeneze taji ambalo utamuvalisha Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki,

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 6:11
18 Referans Kwoze  

Katika maono mengine, Yawe alinionyesha Kuhani Mukubwa Yoshua akisimama mbele ya malaika wa Yawe, na kwa upande wake wa kuume Shetani alisimama kwa kumushitaki.


Umemutimizia mapenzi ya moyo wake; wala haukumukatalia ombi lake.


Mukuje basi enyi wabinti wa Sayuni, mumwone mufalme Solomono. Amevaa taji aliyovalishwa na mama yake, siku alipofanya ndoa yake, siku ambayo moyo wake ulijaa furaha.


Macho yake yalimetameta kama ndimi za moto, na juu ya kichwa chake kulikuwa taji nyingi. Alikuwa na jina lililoandikwa juu yake, wala hakuna mutu aliyejua, isipokuwa yeye mwenyewe tu.


Kisha akawaambia wamuvalishe kitambaa safi juu ya kichwa. Hivyo, wakamuvalisha kitambaa safi na nguo; naye malaika wa Yawe alikuwa akisimama pale.


Katika mwaka wa pili wa utawala wa mufalme Dario wa Persia, siku ya kwanza ya mwezi wa sita, kwa njia ya nabii Hagai, neno la Yawe liliwafikia Zerubabeli mwana wa Saltieli pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki kusema hivi:


Halafu akamuvalisha Haruni kofia na upande wa mbele wa Kofia hiyo akaweka pambo la zahabu, taji takatifu, kama vile Yawe alivyomwamuru.


Kisha wakatengeneza pambo la zahabu safi kwa ajili ya taji takatifu na kuchora juu yake kama vile wanavyochora muhuri: Takatifu kwa Yawe.


Lakini mambo tunayoona ndiyo haya: Yesu alifanywa kuwa mwenye cheo chini kidogo ya malaika kusudi kwa neema ya Mungu, Yesu akufe kwa ajili ya watu wote. Na sasa kwa njia ya kile kifo kilichomufikia, amepata utukufu na heshima.


Basi, Yawe akamutia moyo mutawala Zerubabeli wa Yuda pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua na watu wote waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho. Wakaanza kazi hiyo ya kuijenga upya nyumba ya Yawe wa majeshi, Mungu wao,


Hata hivyo, ujipe moyo, ewe Zerubabeli. –Ni ujumbe wa Yawe. Ujipe moyo, Kuhani Mukubwa Yoshua mwana wa Yosadaki. Mujipe moyo nanyi watu wote wa inchi hii. –Ni ujumbe wa Yawe! Mufanye kazi, maana mimi niko pamoja nanyi. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi!


Yesua mwana wa Yosadaki, pamoja na makuhani wenzake, na Zerubabeli, mwana wa Sealtieli, pamoja na wandugu zake, wakaijenga upya mazabahu ya Mungu wa Israeli, kusudi waweze kumutolea sadaka za kuteketezwa kwa moto kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutu wa Mungu.


Tena utamuvalisha ile kofia juu ya kichwa na kuweka juu ya ile kofia ile taji takatifu.


Niliangalia, nami nikaona farasi mumoja mweupe. Na yule aliyepanda juu yake alikuwa na upindi, akapewa taji. Akatoka akiwa mushindaji na mwenye uwezo wa kuendelea kushinda.


Kisha akatwaa taji ya mufalme wao kutoka kwenye kichwa chake. Uzito wa taji hiyo ya zahabu ulikuwa kilo makumi tatu na tano; na ndani yake mulikuwa jiwe la bei kali. Naye Daudi akavalishwa taji hiyo kwenye kichwa chake. Vilevile aliteka vitu vingi sana katika muji ule.


Hawa ndio makuhani waliooa wanawake wa kigeni: Wazao wa Yesua, wana wa Yehosadaki na wandugu zake: Maseya, Eliezeri, Yaribu na Gedalia.


Taji hiyo italindwa katika hekalu la Yawe kwa heshima ya Heldai, Tobia, Yedaya na Yosia mwana wa Zefania.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite