Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 5:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Yule malaika akaniambia: Mwanamuke yule ni mufano wa uovu! Kisha yule malaika akamusukumia ndani ya kikapu mwanamuke yule na kukifunika.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 5:8
11 Referans Kwoze  

Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Basi mutimize hayo mambo babu zenu waliyoyaanza!


Kikapu chenyewe kilikuwa na mufuniko uliotengenezwa kwa chuma cha risasi; kilifunuliwa, nami nikaona mwanamuke ameikaa mule ndani.


Ninaweza kusema kwamba hawana kosa watu wanaotumia vipimo vya udanganyifu na mawe ya kupimia yasiyokuwa ya kweli?


Aliyahesabu makosa yangu yote akayakusanya pahali pamoja; aliyafunga katika shingo langu kama nira, nikafyonzwa nguvu zangu kwa uzito wake. Yawe aliniweka katika mikono ya watu ambao siwezi kuwapinga.


Mutu mwovu ananaswa kwa uovu wake mwenyewe; anakamatwa na vifungo vya zambi yake mwenyewe.


Hakuna uzima katika mwili wangu, kwa sababu umenikasirikia. Hakuna afya hata katika mifupa yangu, kwa sababu ya zambi yangu.


Wazao wako watarudi hapa katika kizazi cha ine, kwa sababu uovu wa Waamori haujakamilika bado.”


Lakini ninyi mumurudilie Mungu wenu. Mushikamane na wema na haki, mumutumainie Mungu wenu siku zote.


Munajisemesha ndani ya mioyo yenu: Sikukuu ya mwandamo wa mwezi itakwisha wakati gani kusudi tuanze tena kuuzisha vyakula vyetu? Siku ya Sabato itakwisha wakati gani kusudi tupate kuuzisha ngano yetu? Tutapunguza vipimo, tutapandisha bei, tutadanganya watu kwa mizani zisizokuwa sawa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite