5 Yule malaika aliyeongea nami alinikaribia, akaniambia: Inua macho uone kile kinachokuja.
Basi, nikamwuliza: Bwana, farasi hawa wana maana gani? Malaika yule aliyesema nami akaniambia: Nitakuonyesha wale farasi wana maana gani.
Naye akanijibu: Haujui maana ya vitu hivi? Nikamujibu: Sijui bwana wangu.
Kisha, Yawe akanionyesha wafuachuma wane.
Basi, huyo malaika akaniambia: Tangaza kwa sauti na kusema hivi: Yawe wa majeshi anasema hivi: Ninasikia wivu sana juu ya Yerusalema na Sayuni.
Kisha Mungu akaniambia: Wewe mwanadamu, angalia upande wa kaskazini. Nami nikaangalia upande wa kaskazini, na huko upande wa kaskazini wa mulango wa mazabahu, niliona ile sanamu iliyomuchukiza Mungu.