Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 5:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Yawe wa majeshi anasema kwamba yeye mwenyewe ataipeleka laana hiyo. Itapenya kila nyumba ya mwizi na kila nyumba ya mwenye kuapa uongo kwa kutumia jina lake; itakaa mule na kuteketeza nyumba hiyo yote, mbao na mawe.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 5:4
19 Referans Kwoze  

Yawe analaani nyumba za waovu, lakini anabariki makao ya wenye haki.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Nyumba yake tupu, wengine wataishi ndani; kiberiti kimetawanywa katika makao yake.


Musipeleke sanamu zozote katika nyumba zenu, kama sivyo, mutalaaniwa kama sanamu hizo. Muzichukie na kuzizarau kwa sababu ni vitu vilivyolaaniwa.


Hazina zake zitaharibiwa, moto wa ajabu utamuteketeza; kilichobaki katika nyumba yake kitateketezwa.


Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki.


Kama vile mwizi anavyofezeheka anaponaswa, ndivyo Waisraeli watakavyofezeheka; wao wenyewe, wafalme wao, wakubwa wao, makuhani wao na manabii wao.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Kwa hiyo, inchi yote inakauka, wakaaji wake wote wanaangamia pamoja na nyama na ndege; hata samaki wanaangamizwa.


Hawajui kabisa kutenda mambo yanayokuwa sawa! –Ni ujumbe wa Yawe.– Wamejaza nyumba zao nzuri na vitu vya wizi na mateso.


Basi, yeye akaniambia: Ndani ya kitabu hicho kumeandikwa laana ambayo inchi nzima itakayoipata. Upande mumoja imeandikwa kwamba wizi wote watafukuzwa katika inchi, na upande mwingine imeandikwa kwamba wote wenye kuapa uongo watafanyiwa vile vile.


Mutu yeyote asikusudie kumutendea mwenzake ubaya wala musiape uongo, maana ninayachukia sana matendo hayo. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Mutapata laana katika miji yenu na mashamba yenu.


Tutawaacha waishi, kusudi tusipate kuazibiwa kwa sababu ya kiapo tulichofanya.


Wanaegemea nyumba yao lakini haitasimama, wanaishikilia lakini haidumu.


Wale wanaokuchukia watapata haya, makao ya waovu yatatoweka kabisa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite