Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Tena, akaongeza kusema: Mulima huu ni kizuizi? Hapana! Wewe Zerubabeli utausawazisha. Wewe utaanzisha ujenzi mupya wa hekalu, na wakati utakapoliweka jiwe la mwisho, watu watashangilia wakisema: Ni zuri! Kweli, ni zuri!

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 4:7
38 Referans Kwoze  

Mimi ninapingana nawe, ewe mulima muharibifu, mulima unaoharibu dunia nzima! –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitanyoosha mukono wangu juu yako kwa kukuazibu, nitakuangusha kutoka juu kwenye mawe makubwa na kukufanya kuwa mulima uliochomwa kwa moto.


Zerubabeli ameuweka musingi wa hekalu naye vilevile atalikamilisha. Hayo yatakapotukia, watu wangu watajua kwamba mimi Yawe wa majeshi ndimi niliyekutuma kwao.


Kutakuja wakati ambapo mulima wa nyumba ya Yawe utakuwa mukubwa kuliko milima yote. Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote. Watu wengi watakimbilia kule,


Jiwe lililokataliwa na wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.


Milima ilirukaruka kama kondoo dume; vilima vikaruka kama wana-kondoo!


Basi jiwe lile linahesabiwa kuwa la bei kali kwa wale wanaoamini. Lakini kwa wale wasioamini ni: “Jiwe lililotupiliwa na wajengaji, lakini sasa linakuwa jiwe kubwa la pembe.”


Yeye ndiye Maandiko Matakatifu yanayosema hivi juu yake: ‘Jiwe lililokataliwa na ninyi wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.’


Nitawafanya mukuwe kama chombo cha kupepeta, chenye meno mapya na makali. Mutaipepeta milima na kuipondaponda; mutavisagasaga vilima kama maganda.


Enyi milima, mbona muliruka kama kondoo dume? Nanyi vilima, namna gani mumeruka kama mwana-kondoo?


Na ikiwa walichaguliwa kwa neema ya Mungu, si kufuatana na matendo. Ingekuwa vile, neema isingekuwa neema tena.


Milima itayeyuka chini ya miguu yake, kama inta karibu na moto; mabonde yatapasuka, kama vile maji yanayoporomoka kwenye muteremuko.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Visanga vyote vikatoweka na milima haikuonekana tena.


Ninyi vilevile ni kama jengo linalosimama juu ya musingi uliowekwa na mitume na manabii; Yesu Kristo mwenyewe ndiye jiwe kubwa la pembe.


Lakini Yesu akawaangalia na kuwauliza: “Maana ya Maandiko haya Matakatifu ni gani? ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.’


Hivi kila bonde litafunikwa. Kila mulima na kila kilima vitasawanishwa. Njia zenye lukumba zitanyooshwa, nazo njia zenye mashimo zitalainishwa.


Na Yesu akawaambia: “Hamujasoma bado Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji limekuwa jiwe kubwa la musingi. Ni Bwana aliyefanya jambo hili, nalo ni ajabu sana kwetu.’


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Hamujasoma bado Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Jiwe lililokataliwa na wajengaji limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: mukimwamini Mungu pasipo kuwa na shaka, hamutaweza kufanya tu kama nilivyotendea muti huu, lakini vilevile mutaweza kuuambia mulima huu: ‘Ondoka hapa, ujitupe katika bahari,’ na itakuwa vile.


Akisimama dunia inatikisika; akiyatupia mataifa jicho, hayo yanatetemeka. Milima ya milele inavunjwavunjwa, vilima vya zamani za kale vinaanguka; ni juu yao kulipokuwa njia zake za kale na kale.


Wajengaji walipoanza kuweka musingi wa hekalu la Yawe, makuhani wakiwa wamevaa nguo zao, walisimama pahali pao na baragumu katika mikono, nao Walawi wa ukoo wa Asafu wakisimama na matoazi yao, basi, wakamutukuza Yawe kufuatana na maagizo ya mufalme Daudi wa Israeli.


Siku moja tu ndani ya hekalu lako, ni bora kuliko siku elfu pahali pengine; afazali kubakia kwa mulango wa nyumba yako, kuliko kuishi ndani ya nyumba ya waovu.


Neno la Yawe lilinifikia kusema hivi:


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite