Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 4:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Halafu akaniambia: Hawa ndio wale watu wawili ambao Bwana wa ulimwengu wote aliwachagua kwa kuwapakaa mafuta kusudi wamutumikie.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 4:14
28 Referans Kwoze  

Wale washuhuda wawili ndiyo ile miti miwili ya mizeituni na vile vinara viwili vya kuwekea taa vinavyosimama mbele ya Bwana wa dunia.


Kisha uwapakae mafuta kama vile ulivyomupakaa baba yao, kusudi nao vilevile wanitumikie kama makuhani. Kupakwa mafuta huku kutawaingiza katika ukuhani wa kudumu katika vizazi vyao vyote.


Yeye ndiye atakayelijenga hekalu la Yawe. Atapewa heshima ya kifalme na kuikaa kwenye kiti chake cha kifalme kuwatawala watu wake. Kuhani Mukubwa ataikaa karibu na kiti cha kifalme cha mutawala yule, nao wawili watafanya kazi pamoja kwa amani.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Kama vile simba anavyochomoka kutoka ndani ya vichaka vya muto Yordani na kuingia kwenye mbuga, ndivyo nitakavyowafukuza kwa rafla Waedomu toka katika inchi yao. Nami nitamuweka huko mutawala yeyote nitakayemuchagua. Maana, ni nani anayeweza kulinganishwa nami? Nani anayeweza kunishitaki? Ni muchungaji gani anayeweza kunipinga?


Yawe akamwambia Samweli: “Utamulilia Saulo mpaka wakati gani? Wewe unajua kwamba mimi nimemukataa kuwa mufalme wa Israeli. Sasa, jaza ile pembe yako ya kuwekea mafuta, uondoke. Nitakutuma kwa Yese wa muji wa Betelehemu. Maana nimejipatia mufalme kati ya wana wake.”


Halafu Samweli akatwaa chupa ndogo ya mafuta akamumiminia Saulo juu ya kichwa, akamubusu na kumwambia: “Yawe amekutia mafuta ukuwe mutawala juu ya watu wake.


Wakati huo, Yawe akachagua watu wa kabila la Lawi wakuwe wanabeba Sanduku la Agano la Yawe, wamutumikie kama vile makuhani na kubariki watu kwa jina lake hata hivi leo.


Kisha kufanya hivyo, utatwaa yale mafuta ya kupakaa, umumiminie Haruni juu ya kichwa chake kwa kumutakasa.


Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.


Malaika akanijibu: Magari haya ni upepo kutoka pande ine za mbingu. Yalikuwa mbele ya Yawe wa dunia nzima, na sasa yanaondoka.


Muumba wako atakuwa mume wako. Jina lake Yawe wa majeshi. Mukombozi wako ni Mutakatifu wa Israeli. Yeye anaitwa Mungu wa Ulimwengu Wote.


Nitaimba juu ya rafiki yangu, wimbo wa rafiki yangu na shamba lake la mizabibu: Rafiki yangu alikuwa na shamba la mizabibu juu ya kilima chenye udongo muzuri.


Yawe amekuapia hivi wala hatabadilisha nia yake: “Wewe ni kuhani milele kwa utaratibu wa ukuhani wa Melkisedeki.”


Zamani ulisema katika maono, ukawaambia watumishi wako waaminifu: “Nimemupa nguvu shujaa mumoja, nimemwinua huyo niliyemuchagua kati ya watu.


“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Wakati miguu ya makuhani wanaobeba Sanduku la Agano la Yawe, Bwana wa dunia yote, itakapoingia katika maji ya muto Yordani, maji ya muto huo yataacha kutiririka. Na yale yatakayokuwa yanatiririka kutoka upande wa juu yatajikusanya pamoja kama lundo.”


Muangalie, Sanduku la Agano la Bwana wa dunia yote liko karibu kupita mbele yenu kuelekea muto Yordani.


Vilevile Musa akamupakaa Haruni mafuta juu ya kichwa kwa kumutakasa.


Nao Zerubabeli mwana wa Saltieli, na Yesua mwana wa Yosadaki, walipousikia ujumbe huo wakaanza tena kuijenga nyumba ya Mungu katika Yerusalema, wakisaidiwa na manabii wa Mungu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite