Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 3:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Mukumbuke kwamba nimeweka mbele ya Yoshua jiwe moja lenye nyuso saba. Nami nitachora maandiko juu yake, na kwa siku moja tu, nitaiondoa zambi ya inchi hii. Kweli, ni mimi Yawe wa majeshi ninayesema hivyo.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 3:9
34 Referans Kwoze  

Maendeleo ya ujenzi wa hekalu yanaonekana madogo, na watu wanayazarau; lakini watamwona Zerubabeli akiendelea kulijenga hekalu, nao watafurahi. Sasa, juu ya hizo taa saba, yule malaika akaniambia: Ni macho saba ya Yawe yanayoona kila nafasi katika dunia.


Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Halafu nikaona Mwana-Kondoo akisimama katikati ya kiti cha kifalme chenye kuzungukwa na vile viumbe vine vya ajabu na wale wazee, naye alionekana kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba; ndizo roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote.


Basi, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Ninaweka katika Sayuni jiwe la musingi, jiwe ambalo limeimarishwa. Jiwe la pembe, la bei kali, jiwe ambalo ni la musingi imara; jiwe linalokuwa na maandiko haya: Anayeamini hataanguka.


Jiwe lililokataliwa na wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.


kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Angalia, ninaweka jiwe la kukwalisha katika Sayuni nalo ni la kuangusha. Lakini yule anayemwamini hatapata haya.”


Wala hawatafundishana tena kila mutu na jirani yake, na kila mutu na ndugu yake na kusema “Mumujue Yawe”, kwa sababu wote, wadogo kama vile wakubwa, watanijua mimi Mungu. Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena zambi zao.


Yeye hahitaji kutoa sadaka kila siku kama vile Makuhani wengine Wakubwa, kwanza kwa ajili ya zambi zake mwenyewe na kisha kwa ajili ya zambi za watu. Kwa maana amefanya vile mara moja tu wakati alipojitoa mwenyewe kufa.


Lakini musingi uliojengwa na Mungu, unasimama imara. Nayo maneno haya yamechapwa juu ya musingi ule “Bwana anajua wale wanaokuwa wake,” na haya mengine: “Kila mutu anayesema kwamba yeye ni wa Bwana anapaswa kujitenga na maovu.”


Ameweka kitambulisho juu yetu kinachohakikisha kama sisi ni watu wake na kuweka Roho Mutakatifu ndani yetu kuwa rehani ya vitu vyote anavyotuwekea.


Yeye ndiye sadaka iliyotolewa kwa ajili ya usamehe wa zambi zetu, wala si kwa ajili ya zambi zetu tu, lakini kwa ajili ya zambi za watu wote.


Inaonekana wazi kwamba ninyi ni barua iliyoandikwa na Kristo na kutumwa kwa njia ya utumishi wetu. Barua hii inaandikwa si kwa wino, lakini kwa Roho wa Mungu Mwenye Uzima. Barua hiyo haikuandikwa juu ya vibao vya mawe, lakini katika mioyo ya watu.


Yeye ndiye Maandiko Matakatifu yanayosema hivi juu yake: ‘Jiwe lililokataliwa na ninyi wajengaji, limekuwa sasa jiwe kubwa la musingi.’


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Malaika akawaambia watumishi wake: Muvue Kuhani Mukubwa Yoshua nguo zake zenye kuchafuka. Kisha akamwambia Kuhani Mukubwa Yoshua: Nimeiondoa zambi yako, nami nitakupatia nguo za bei kali.


Yawe anachunga kwa uangalifu ulimwengu wote, kwa kuwapa nguvu wale wanaokuwa waaminifu kwake. Umetenda jambo la kipumbafu, kwa hiyo tangu sasa, utakuwa na vita kila mara.”


Kisha, utatengeneza bamba la zahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile mutu anavyochora muhuri: Takatifu kwa ajili ya Yawe.


Basi, kutakuwa mawe kumi na mawili yaliyochorwa majina kumi na mawili ya wana wa Israeli. Kila moja litakuwa kama muhuri, kwa kusimamia makabila yale kumi na mawili.


Utayachora majina yale juu ya yale mawe kama vile muchoraji anavyochora muhuri, kisha uyaingize katika kingo za zahabu.


Kama mashariki inavyokuwa mbali na magaribi, ndivyo anavyotenga zambi zetu mbali nasi.


Na sasa, bwana wangu mufalme, Waisraeli wote wanakungojea, kusudi uwaambie yule atakayeikaa juu ya kiti chako nyuma yako, bwana wangu mufalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite