Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 3:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukifuata njia zangu na kushika maagizo niliyokupa, basi, utaisimamia nyumba yangu na viwanja vyake. Nami nitakuwezesha kuingia katika utumishi wangu kama hawa wanaosimama mbele yangu.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 3:7
30 Referans Kwoze  

kwa sababu Abrahamu alinitii mimi, akashika maagizo yangu, amri zangu, masharti yangu na sheria zangu.”


Yesu akawajibu: “Kweli ninawaambia: Katika ulimwengu mupya, Mwana wa Mutu atakapoikaa juu ya kiti chake cha kifalme chenye utukufu, ninyi kumi na wawili mulionifuata mutaikaa vilevile juu ya viti kumi na viwili vya kifalme kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.


Mutabaki kwenye mulango wa hema la mukutano usiku na muchana kwa muda wa siku saba, mukifanya mambo Yawe aliyoamuru, kama sivyo mutakufa. Ndivyo nilivyoamuriwa na Yawe.


Yule atakayeshinda, nitamwikalisha karibu nami kwenye kiti changu cha kifalme, kama vile mimi nilivyoshinda na kuikaa karibu na Baba yangu kwenye kiti chake cha kifalme.


Ndani ya nyumba ya Baba yangu kuna nafasi nyingi za kukaa. Isingekuwa hivi singewaambia kwamba ninakwenda kuwatayarishia nafasi.


kusudi mupate kula na kunywa pamoja nami katika ufalme wangu. Mutaikaa vilevile juu ya viti vya kifalme, kwa kuhukumu makabila kumi na mawili ya Waisraeli.”


Malaika akanijibu: Magari haya ni upepo kutoka pande ine za mbingu. Yalikuwa mbele ya Yawe wa dunia nzima, na sasa yanaondoka.


Halafu akaniambia: Hawa ndio wale watu wawili ambao Bwana wa ulimwengu wote aliwachagua kwa kuwapakaa mafuta kusudi wamutumikie.


Eneo hilo litakuwa kwa ajili ya makuhani wa uzao wa Zadoki, ambao walinitumikia kwa uaminifu na hawakuasi wakati Waisraeli walipoasi kama Walawi walivyofanya.


Kwa hiyo, ilikuwa ni kazi yao kutunza hema la kusanyiko na Pahali Patakatifu, na kuwasaidia wandugu zao makuhani, wazao wa Haruni, kwenye ibada katika nyumba ya Yawe.


Timiza maagizo ya Yawe, Mungu wako, ufuate njia zake na kushika masharti yake, amri zake, maagizo yake na maamuzi yake kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa. Kwa hiyo, utafanikiwa katika kila jambo unalofanya na kokote unakoenda.


Kisha kutimiza kazi ya vitu vyangu vitakatifu, mumeruhusu watu wa mataifa mengine kutimiza kazi hiyo katika hekalu langu.


Kwa hiyo, Musa akamwambia Haruni: Kwa tukio hili Yawe amekuonyesha maana ya kile alichosema: Nitajionyesha kuwa mutakatifu kati ya wale wanaokuwa karibu nami, nitatukuzwa mbele ya watu wote! Haruni akanyamaza kimya.


Tena kama ukifuata njia yangu na kushika masharti na amri zangu kama vile baba yako Daudi alivyofanya, basi, nitakupa maisha marefu.”


Lakini ninyi muliovuna ngano hiyo, mutaikula na kunitukuza mimi Yawe. Ninyi muliochuma mizabibu hiyo, mutakunywa divai yake katika viwanja vya hekalu langu takatifu.


Malaika wa Yawe akamwonya Kuhani Mukubwa Yoshua, akamwambia:


Watu wanaokaa katika inchi za mbali watakuja kusaidia kwa kulijenga hekalu langu mimi Yawe. Nanyi mutajua kwamba Yawe wa majeshi, ndiye aliyenituma kwenu. Haya yote yatatukia kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite