Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 3:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Malaika akawaambia watumishi wake: Muvue Kuhani Mukubwa Yoshua nguo zake zenye kuchafuka. Kisha akamwambia Kuhani Mukubwa Yoshua: Nimeiondoa zambi yako, nami nitakupatia nguo za bei kali.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 3:4
34 Referans Kwoze  

Lakini baba yake akawaambia watumishi wake: ‘Mulete mbio kanzu nzuri sana na kumuvalisha nayo. Mumuvalishe pete kwenye kidole chake na mumuvalishe viatu.


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Lakini mimi ndiye niliyefuta makosa yenu kwa heshima yangu, ndiye ninayefuta makosa kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka zambi zenu.


Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Ukifuata njia zangu na kushika maagizo niliyokupa, basi, utaisimamia nyumba yangu na viwanja vyake. Nami nitakuwezesha kuingia katika utumishi wangu kama hawa wanaosimama mbele yangu.


Ee Mungu, ni nani anayekuwa kama wewe? Wewe unasemehe zambi za watu wako waliobaki, wala hauyaangalii makosa yao. Hasira yako haidumu milele, lakini unapendelea zaidi kutuonyesha wema wako.


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Mimi nitawasamehe maovu yao, wala sitakumbuka tena zambi zao.”


Kwa maana Kristo alikuwa bila zambi, lakini Mungu alimubebesha muzigo wa zambi zetu, kusudi kwa njia yake tupate kuwa wenye haki mbele ya Mungu.


Mukumbuke kwamba nimeweka mbele ya Yoshua jiwe moja lenye nyuso saba. Nami nitachora maandiko juu yake, na kwa siku moja tu, nitaiondoa zambi ya inchi hii. Kweli, ni mimi Yawe wa majeshi ninayesema hivyo.


Unitakase kwa hisopo, nikuwe safi, unisafishe, nikuwe mweupe pee.


na kuvaa utu mupya. Utu ule unaendelea kufanywa upya kila mara kufuatana na mufano wa Mungu anayekuwa muumba wake, kusudi mupate kumujua hakika.


Kwa maana mushahara wa zambi ni kifo, lakini zawadi Mungu anayotoa ni uzima wa milele kwa kuungana na Yesu Kristo, Bwana wetu.


kuhesabiwa haki na Mungu kunapatikana kwa njia ya imani katika Yesu Kristo kwa wote wanaoamini, kwa maana hakuna tofauti yoyote kati yao,


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Malaika akamujibu: “Mimi ni Gabrieli, anayebaki karibu na Mungu! Nimetumwa kusema nawe, kwa kukuletea habari hii njema.


Katika maono mengine, Yawe alinionyesha Kuhani Mukubwa Yoshua akisimama mbele ya malaika wa Yawe, na kwa upande wake wa kuume Shetani alisimama kwa kumushitaki.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Kisha Mikaya akasema: “Sasa sikia neno la Yawe: Nilimwona Yawe akiikaa katika kiti chake cha kifalme, na jeshi lote la mbinguni likisimama pembeni yake, upande wake wa kuume na wa kushoto.


Basi, Daudi akamwambia Natani: “Nimetenda zambi mbele ya Yawe.” Natani akamwambia: “Yawe amekusamehe zambi yako, nawe hautakufa.


Kisha nikaangalia tena, nikasikia sauti ya wamalaika wengi wenye kuzunguka kiti cha kifalme, na viumbe vya ajabu na wazee. Hesabu yao ilikuwa maelfu na maelfu na mamilioni na mamilioni.


“Naye mufalme alipoingia kwa kuwaangalia wale wageni, akamwona mutu mumoja asiyevaa nguo ya karamu.


Makuhani ambao watakuwa wakitumika katika Pahali Patakatifu, wanapotaka kwenda kwenye kiwanja cha inje, ni lazima waache humo nguo zao walizovaa walipokuwa wanatumika mbele ya Yawe kwa sababu nguo hizo ni takatifu. Ni lazima wavae nguo zingine mbele ya kutoka inje ambako watu wanakusanyika.


Utatuhurumia tena; utatupilia mbali zambi zetu, utazitupa zote katika vilindi vya bahari.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Basi, Yoyakinu alibadilisha nguo zake za wafungwa, akakuwa anapata chakula chake siku zote kwenye meza ya mufalme.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite