Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 2:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi, huyo malaika aliyezungumuza nami akamwambia yule mwenzake: Kimbia umwambie yule kijana kwamba si lazima Yerusalema ukuwe na kuta, kama sivyo hapatakuwa nafasi ya kuwatoshelea wakaaji wake wengi na nyama watakaokuwa ndani yake.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 2:8
50 Referans Kwoze  

Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche chini ya kivuli cha mabawa yako,


Yawe alikuta Waisraeli katika inchi ya jangwa, jangwa tupu zenye upepo mukali. Aliwalinda na kuwatunza. Aliwakinga kama mboni ya jicho lake.


Lakini Musaidizi, ndiye Roho Mutakatifu, yule Baba atakayemutuma kwa jina langu, atawafundisha maneno yote na kuwakumbusha yote niliyowaambia.


Kwa maana, Mungu yuko na haki ya kuwatesa wale wanaowatesa ninyi,


Mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokitendea mumoja wa hawa wandugu zangu wanaohesabiwa kuwa wadogo, mulinitendea mimi.’


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Kama vile ulivyonituma katika dunia, mimi vilevile nimewatuma katika dunia.


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


Nimeyasikia matusi ya Wamoabu na mazarau ya Waamoni, jinsi walivyowatusi watu wangu na kujivuna kwamba wamenyanganya inchi yao.


Wewe umenyanganya mataifa mengi, lakini wote wanaobaki watakunyanganya wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima wataenea kati ya mataifa mengi, watakuwa kama umande unaotoka kwa Yawe, kama manyunyu yanayoanguka kwenye majani ambayo hayasababishwi na mutu wala kumutegemea mwanadamu.


Mataifa mengi yamekusanyika kwa kuwashambulia. Yanasema: Muache muji wao uchafuliwe, nasi tufurahie kuona uharibifu wa Sayuni!


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Edomu, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamewawinda wandugu zao Waisraeli kwa mapanga, wakaitupilia mbali huruma yao yote ya kindugu. Hasira yao haikuwa na mwisho, waliiacha iwake siku zote.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Tiro, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Wamekamata watu wengi na kuwapeleka mpaka Edomu. Hawakutii mapatano ya urafiki waliokuwa wamefanya.


Ulikuwa adui wa siku zote wa Waisraeli, ukasababisha watu wake wauawe kwa upanga, wakati wa musiba wao, wakati wa azabu yao ya mwisho.


Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kwa sababu Wafilistini walifanya kisasi, wakawalipiza kisasi waadui zao kwa ubaya sana na kuendelea kuwa waadui zao siku zote,


Bwana wetu Yawe alisema hivi: Kwa sababu Waedomu wamefanya kisasi na Yuda, wakawalipiza watu wa Yuda kisasi kibaya sana


Basi, Yawe akamupelekea makundi ya Wababeli, Waaramu, Wamoabu na Waamoni washambulie inchi ya Yuda na kuiharibu, kulingana na neno la Yawe alilolisema kwa njia ya watumishi wake manabii.


Basi, Mungu akamwambia katika hiyo ndoto: “Sawa. Ninajua kwamba umefanya hivyo kwa moyo safi. Mimi ndiye niliyekuzuia kutenda zambi mbele yangu. Ndiyo maana sikukuruhusu umuguse huyo mwanamuke.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Yawe anasema kwamba yeye mwenyewe atakuwa ukuta wa moto kwa kuulinda muji huo pande zote, naye atakaa mule kwa utukufu wake.


Naye mufalme atawajibu: ‘Kweli ninawaambia: kila kitu mulichokosa kumutendea mumoja wa hawa wanaohesabiwa kuwa wadogo, hamukunitendea mimi.’


Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia: “Saulo, Saulo, sababu gani unanitesa?”


Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe; uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha. Yote hayo yatakupata wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Ufuate amri zangu nawe utaishi; ulinde mafundisho yangu kama mboni ya jicho lako.


Yawe anasema hivi juu ya jirani wabaya za watu wake: Wamegusa sehemu ya urizi wangu, niliowapatia watu wangu Waisraeli! Basi nitawaongoa kutoka katika inchi yao, na hata watu wa Yuda nitawaongoa katika inchi yao.


Mataifa yote yatamutumikia yeye, pamoja na mwana wake na mujukuu wake mpaka wakati inchi yake itakapoanguka. Kisha mataifa mengi na wafalme wengi wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.


Nitakuteremusha ndani ya shimo kusudi ujiunge na wale wanaokuwa huko, walioishi zamani katika dunia; utakaa kule katika matongo kwa milele. Hautakaliwa na watu milele na hautakuwa na nafasi katika inchi za wanaokuwa wazima.


Kwa hiyo, ewe mwanadamu, toa unabii na kumwambia Gogi kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Siku ile, taifa langu la Waisraeli litaishi kwa usalama, wewe utafunga safari


Kweli umepatwa na uharibifu, makao yako yamekuwa matupu, na inchi yako imeteketezwa. Lakini sasa itakuwa ndogo sana kwa wakaaji wake.


Nitawafanya watu na nyama waongezeke na kuwa wengi. Nitawafanya ninyi milima mukaliwe tena kama zamani. Nitawatendea mema mengi kuliko zamani. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Nitakwenda kuishambulia inchi isiyokuwa na kuta, inchi ambako wanainchi wake wanaishi kwa amani. Wote wanakaa katika miji isiyokuwa na kuta; hawana vifungio wala milango.


Barabara za Yerusalema zitajaa vijana wanaume na wanawake, wakichezacheza mule.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite