Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.
Kisha nikasikia sauti ingine kutoka mbinguni ikisema: “Mutoke katika muji ule ninyi watu wangu, kusudi musishiriki zambi zake na kupatwa vilevile na mapigo yatakayoupata.
Mukimbie kutoka Babeli, kila mutu apate kuyaokoa maisha yake! Musiangamizwe katika azabu yake, maana huu ndio wakati wa Mungu wa kulipiza kisasi, anaiazibu Babeli kama inavyostahili.
Walipowatosha inje ya muji, malaika mumoja wao akawaambia: “Mukimbie kwa ajili ya usalama wenu. Musiangalie nyuma wala kusimama popote katika bonde. Mukimbilie kwenye milima, musipate kuangamia.”
Enyi watu wa Sayuni, mulie na kugaagaa kama mwanamuke anayezaa! Maana sasa mutaondoka katika muji huu muende kukaa katika mbuga, mutakwenda mpaka Babeli. Lakini kule, mutaokolewa. Kule Yawe atawakomboa toka katika makucha ya waadui zenu.
Alipofika, akawaambia watu: Tafazali muondoke kwenye hema za watu hawa waovu na musiguse kitu chao chochote, musiangamizwe pamoja nao kwa sababu ya zambi zao zote.
Shuka, uikae katika mavumbi, ewe bikira, binti wa Babeli! Ikaa chini pasipo kiti cha kifalme, ewe binti wa Wakaldea! Tokea sasa hautaitwa tena murembo wala mwenye kupendeza.