Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 2:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 2:5
28 Referans Kwoze  

Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote.


Wengi wanasema juu yangu: “Hautapata musaada wowote kwa Mungu.”


Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.


Muji ule hauna lazima ya mwangaza wa jua, wala wa mwezi, kwa sababu utukufu wa Mungu unauangazia na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Sayuni, mulima wa Mungu, unapendeza kwa urefu; muji wa Mufalme mukubwa ni furaha ya ulimwengu.


Humo Yawe atatuonyesha ukubwa wake. Kutakuwa mito mikubwa na vijito, lakini mashua za vita hazitapita, wala mashua kubwa kuingia.


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Watu wa Sayuni wafurahi! Watu wa Yuda washangilie, kwa sababu ya hukumu yako ya haki!


Kuna muto ambao maji yake yanafurahisha muji wa Mungu, makao matakatifu ya Mungu Mukubwa.


Ninasikiliza yale Yawe anayosema, maana anaahidi kuwapa watu wake amani, watu wake mwenyewe wasiporudilia upumbafu wao.


Kama vile milima inavyozunguka Yerusalema, ndivyo Yawe anavyozunguka watu wake, tangu sasa na hata milele.


Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu, na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga. –Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.


Watu wangu watakaa katika makao ya amani, katika pahali penye usalama na nafasi yenye utulivu.


Kwa hiyo, ewe mwanadamu, toa unabii na kumwambia Gogi kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Siku ile, taifa langu la Waisraeli litaishi kwa usalama, wewe utafunga safari


Hivyo akakuwa amepima pande zote, nazo zilikuwa metre mia mbili makumi tano kila upande. Ukuta huo ulitenganisha kati ya eneo takatifu na lile la kawaida.


Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


Nayo kamba ya kupima itanyooshwa moja kwa moja mpaka kwenye mulima Garebu, kisha itazungushwa mpaka Goa.


Yule mutu akapima kwa ufito wake, akapima metre mia tano kwenda chini upande wa mashariki, akanipitisha kwenye maji. Maji yalifika kwenye miguu tu.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite