Halafu, kila pahali juu ya mulima Sayuni na juu ya mikutano ya watu atafanya kuwe wingu wakati wa muchana, na moshi na moto unaowaka vizuri wakati wa usiku. Zaidi ya hayo utukufu wa Mungu utaufunika na kuulinda muji wote.
Mufalme wao atatoroka kwa ajili ya hofu, na wakubwa wao wataiacha bendera yao kwa ajili ya woga. –Ni ujumbe wa Yawe ambaye moto wake uko katika Sayuni, ambaye furu lake liko katika Yerusalema.
Kwa hiyo, ewe mwanadamu, toa unabii na kumwambia Gogi kwamba Bwana wenu Yawe anasema hivi: Siku ile, taifa langu la Waisraeli litaishi kwa usalama, wewe utafunga safari
Hivyo akakuwa amepima pande zote, nazo zilikuwa metre mia mbili makumi tano kila upande. Ukuta huo ulitenganisha kati ya eneo takatifu na lile la kawaida.
Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.