Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 2:4
24 Referans Kwoze  

Kisha malaika yule akaniambia nitangaze ujumbe huu mwingine: Yawe wa majeshi anasema hivi: Miji yake itafurika tena na fanaka. Yawe atafariji tena Sayuni, atachagua Yerusalema kuwa wake.


Siku inakuja ambapo kuta za muji wenu zitajengwa upya. Siku hiyo mipaka ya inchi yenu itapanuliwa.


Nitakwenda kuishambulia inchi isiyokuwa na kuta, inchi ambako wanainchi wake wanaishi kwa amani. Wote wanakaa katika miji isiyokuwa na kuta; hawana vifungio wala milango.


Kama vile nyota katika anga na muchanga katika bahari visivyoweza kuhesabiwa, ndivyo nitakavyoongeza hesabu ya wazao wa mutumishi wangu Daudi na hesabu ya makuhani wa ukoo wa Lawi.


Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.


Siku zinakuja ambapo nitaijaza inchi ya Israeli na inchi ya Yuda watu na nyama kama vile mulimaji anavyopanda mbegu.


Watoto wako waliozaliwa katika uhamisho, watakulalamikia wakisema: Inchi hii ni ndogo sana; utupatie nafasi zaidi ya kuishi.


Lakini ninahakikisha ujumbe wa mutumishi wangu, na kukamilisha mipango ya wajumbe wangu. Mimi ndiye ninayesema juu ya Yerusalema: Wewe Yerusalema, watu watakaa ndani yako tena. Na juu ya miji ya Yuda: Ninyi mutajengwa tena: mabomoko yenu yatatengenezwa tena.


Halafu watu wa Yuda na miji yake yote, walimaji na wachungaji wanaopitapita na makundi yao watakaa huko pamoja.


Muangalie Sayuni tunamofanyia sikukuu zetu; muangalie Yerusalema, makao matulivu, hema imara; misumari yake haitaongolewa hata kidogo, kamba zake hazitakatwa hata moja.


Usijiachilie kuzarauliwa na mutu yeyote kwa sababu ungali bado kijana. Lakini ukuwe mufano kwa waamini, katika masemi yako, katika mwenendo wako, katika upendo, katika imani na katika maisha safi.


Mungu aliwajalia vijana wale wane maarifa na ujuzi katika elimu na hekima. Zaidi ya hayo, alimujalia Danieli ufahamu wa kufasiria maono na ndoto.


Nami nikajibu: Ee! Bwana wangu Yawe, mimi sijui kusema, ningali bado kijana.


Kutokana na sababu hii, Wayuda wanaokaa katika vijiji na katika miji midogo wanasherehekea siku ya kumi na ine ya mwezi wa Adari kuwa sikukuu ya furaha, na kupelekeana zawadi wakati wale wanaoishi katika miji mikubwa wanasherehekea siku ya kumi na tano ya mwezi wa Adari kama siku ya mapumziko, na kupelekeana vilevile zawadi.


Mufalme alitaka vijana wasiokuwa na kilema, wazuri kwa umbo, wenye ujuzi wa kila hekima, wenye akili na maarifa na wanaofaa kwa kutumika katika nyumba ya kifalme. Alitaka vilevile vijana wale wafundishwe kusoma na kuandika luga ya Wakaldea.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.


Mimi ndiye niliyemwumba mufuaji wa vyuma, anayewasha moto wa makaa na kufua silaha. Ni mimi vilevile niliyemwumba mwangamizaji anayeangamiza.


Lakini juu ya wale watu ambao walikuja kupigana na Yerusalema, hizi ndizo hasara ambazo Yawe atawaletea: Miili yao itaoza wangali wazima; macho yao yataoza yakiwa kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza zikiwa katika vinywa vyao.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite