Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 2:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kweli, nitawashambulia wale waliowakamata mateka, nao watakamatwa mateka na wale waliowafanya watumwa wao. Halafu kwa hiyo mutajua kwamba Yawe wa majeshi ndiye aliyenituma.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 2:13
26 Referans Kwoze  

Lakini Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; dunia yote ikae kimya mbele yake.


Munyamaze mbele ya Bwana wenu Yawe, maana siku ya Yawe iko karibu. Yawe ametayarisha sadaka, naye amekwisha kutakasa waalikwa wake.


Mumwimbie Mungu, musifu jina lake; mumutengenezee njia yeye anayetembea juu ya mawingu. Jina lake ni Yawe; mufurahi mbele yake.


Kwa hiyo muningojee mimi Yawe, ngoja siku nitakaposimama kutoa mashitaki. Nimeamua kuyakusanya mataifa na falme, kuyamwangia kasirani yangu, na ukali wa hasira yangu. Dunia yote itateketezwa kwa moto wa kasirani yangu.


Kisha Bwana aliamuka kama kutoka katika usingizi, kama shujaa aliyechangamushwa na divai.


Halafu sasa wewe mwanadamu ni nani hata ubishane na Mungu? Chombo cha udongo hakiwezi kumwuliza mufinyanzi: “Kwa nini umenitengeneza hivi?”


Amuka! Amuka na nguvu, ee mukono wa Yawe! Amuka kama ulivyofanya hapo zamani, nyakati za vizazi vilivyopita. Si wewe ndiwe uliyemukatakata yule nyama mukubwa Rahabu, ukamutoboa yule nyoka mukubwa wa kuogopesha?


Anakomesha vita popote katika dunia. Anavunjavunja pinde na mikuki, nayo magari ya vita anayateketeza.


Yawe yuko katika hekalu lake takatifu; kiti cha kifalme cha Yawe kiko mbinguni. Kwa macho yake anawachungulia wanadamu, na kujua kila kitu wanachofanya.


Uangalie chini kutoka makao yako matakatifu mbinguni, uwabariki watu wako Israeli na inchi uliyotupatia kama vile ulivyowaapia wazee wetu; inchi inayotiririka maziwa na asali’.


Basi tunajua kama maneno yote yanayosemwa na Sheria, yanawaelekea wale wanaolazimishwa kutii Sheria, kusudi mutu yeyote asikuwe na namna ya kujitetea, na dunia nzima ipaswe kuhukumiwa na Mungu.


Basi, wewe Yeremia utatabiri maneno haya yote juu yao, na kusema hivi: Yawe atanguruma kutoka juu, atatoa sauti yake kutoka kwenye makao yake matakatifu; atanguruma kwa nguvu kwa ajili ya watu wake, atapiga kelele kama wenye kukamua zabibu, kwa ajili ya wakaaji wote wa dunia.


Utuchungulie kutoka mbinguni, ee Mungu, uone, utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu. Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako? Hatuoni tena upendo na huruma yako.


Hivi ndivyo anavyosema Mungu anayekuwa juu kabisa, anayeishi milele na ambaye jina lake ni Mutakatifu: Mimi ninakaa kule juu, Pahali Patakatifu, ninakaa vilevile na wenye majuto na wanyenyekevu. Mimi nitawatia moyo wanaokuwa wanyenyekevu na kuwapa nguvu wenye majuto.


Ninyi munawaka tamaa kwenye miti ya mialo, na chini ya kila muti wenye kuwa na majani mabichi. Munawachinja watoto wenu na kuwatambikia katika mabonde na ndani ya nyufa za mawe.


Kisha, makuhani na Walawi wakawaombea watu baraka za Yawe, naye katika makao yake matakatifu kule mbinguni akasikia maombi yao na kuyakubali.


Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.


“Lakini ninyi munaweza kusema: ‘Tutaweza namna gani kutambua neno ambalo Yawe hakulisema?’


Kama nabii akisema kitu aseme ni kwa jina la Yawe, na kitu hicho hakifanyiki au hakiko kweli, jambo hilo Yawe hakulisema; nabii amelisema kwa kiburi, nanyi musitishwe na jambo hilo.


Watu wa mataifa watawasaidia Waisraeli kurudi katika inchi waliyopewa na Yawe. Na hapo watawatumikia Waisraeli kama watumwa. Wale waliowateka sasa watatekwa na Waisraeli, na watawatawala wale waliowatesa.


Siku ile watu wa Misri wataogopa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu watakapomwona Yawe wa majeshi ameunyoosha mukono wake juu yao.


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.


Zerubabeli ameuweka musingi wa hekalu naye vilevile atalikamilisha. Hayo yatakapotukia, watu wangu watajua kwamba mimi Yawe wa majeshi ndimi niliyekutuma kwao.


Watu wanaokaa katika inchi za mbali watakuja kusaidia kwa kulijenga hekalu langu mimi Yawe. Nanyi mutajua kwamba Yawe wa majeshi, ndiye aliyenituma kwenu. Haya yote yatatukia kama mukiitii sauti ya Yawe, Mungu wenu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite