ZAKARIA 2:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
12 Yawe wa majeshi, ambaye kwa utukufu wake amenituma, anasema hivi juu ya mataifa yaliyowakamata mateka watu wake: Hakika, anayewagusa ninyi anagusa mboni ya jicho langu.
Kisha malaika yule akaniambia nitangaze ujumbe huu mwingine: Yawe wa majeshi anasema hivi: Miji yake itafurika tena na fanaka. Yawe atafariji tena Sayuni, atachagua Yerusalema kuwa wake.
Lakini Mungu wa Yakobo si kama sanamu hizo, maana, yeye ndiye aliyeumba vitu vyote, na Israeli ni taifa linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.
Mungu anayekuwa hazina ya Yakobo si kama hizo, maana yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote, na Israeli ni kabila linalokuwa mali yake; Yawe wa majeshi, ndilo jina lake.
wewe niliyekuleta toka miisho ya dunia, niliyekuita toka mbali kwa mipaka ya dunia, wewe niliyekuambia: Wewe ni mutumishi wangu; mimi sikukutupilia, lakini nilikuchagua.
Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.
Malaika wa Yawe akamwambia yule Shetani: Yawe akulaani, ewe Shetani! Kweli, Yawe aliyechagua Yerusalema akulaani! Huyu ni kama kipande cha kuni kilichoopolewa ndani ya moto!
Kule akawaelezea Zeresi, muke wake, na warafiki zake wote mambo yote yaliyomupata. Zeresi na hao warafiki zake wakamwambia: “Ikiwa huyu Mordekayi, ambaye umeanza kupoteza madaraka yako kwa ajili yake ni wa kabila la Wayuda, basi, hautamuweza; atakushinda kabisa.”
Lakini wote wanaokuangamiza, wataangamizwa vilevile, na waadui zako wote watapelekwa katika uhamisho; nao wanaokukamata mateka watakamatwa mateka, nao wanaokuwinda, nitawawinda.