Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 2:11
36 Referans Kwoze  

Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


“Na kwa kumaliza, basi mujue kwamba habari ya wokovu huu wa Mungu imetumwa kutangazwa kwa watu wa mataifa mengine, nao wataisikia!” [


Ndio utakaowaangazia mataifa, na kuleta utukufu kwa watu wako Waisraeli.”


Yawe anasema hivi: Utajiri wa Misri na faida ya uchuuzi za Kushi, pamoja na za watu wa Seba, wale watu warefu sana, zitakuja kwako mwenyewe wewe taifa la Israeli, zote zitakuwa mali yako. Watu hao watakufuata wakifungwa minyororo; watainama mbele yako na kukusihi wakisema: Kwako kuna Mungu wa kweli, wala hakuna Mungu mwingine lakini yeye.


Ninaomba kusudi wote wakuwe mumoja, kama vile wewe Baba unavyokuwa ndani yangu na mimi ndani yako. Ninaomba vilevile kwamba wakuwe ndani yetu, kusudi dunia ipate kuamini kwamba umenituma.


Watu wa mataifa katika dunia yote tokea upande jua linapopanda mpaka upande jua linaposhuka wanalitukuza jina langu. Kila pahali wananifukizia ubani na kunitolea sadaka zinazokubaliwa; maana jina langu linatukuzwa kati yao.


Siku hiyo, kila mumoja wenu atamwalika mwenzake kufurahia amani na utulivu katika shamba lake la mizabibu na la tini.


Lakini hayo unayosema yatakapotukia –nayo kweli yatatukia –basi, halafu watatambua kwamba nabii amekuwa kati yao.


Ee Yawe! Wewe ndiwe nguvu yangu na upango wangu; wewe ni kimbilio langu wakati wa taabu. Mataifa toka pande zote za dunia yatakufikia na kusema: Miungu ya babu zetu ilikuwa ya uongo, ilikuwa ya bure, isiyofaa kitu.


Nitaweka kati yao kitambulisho cha uwezo wangu. Watakaookolewa kati yao nitawapeleka kwa watu wa mataifa kule Tarsisi, Puti, Ludi, inchi zenye wafundi wa kupiga upinde; watakwenda vilevile Tubali na Ugriki na katika visanga vya mbali ambapo watu hawajapata kusikia habari zangu wala kuuona utukufu wangu. Wale wajumbe wangu watautangaza utukufu wangu katika mataifa hayo.


Yawe ameonyesha nguvu yake tukufu, mbele ya mataifa yote. Atawaokoa watu wake, na ulimwengu wote utashuhudia.


Jina la mufalme litukuzwe siku zote; utukufu wake udumu muda wote jua litakapokuwa. Kwake mataifa yote yabarikiwe; watu wote wamwite mwenye heri!


Baba mwenye haki, ijapokuwa dunia haikujui, mimi ninakujua na hawa wanajua kwamba ulinituma.


Ninaomba nikuwe ndani yao na wewe ndani yangu, kusudi wapate kuwa mumoja kabisa; na dunia ijue kama wewe ndiwe uliyenituma na kwamba unawapenda kama vile unavyonipenda.


Sheria zilezile zitaelekea Mwisraeli aliyezaliwa katika inchi na wageni watakaoishi kati yenu.”


Musogee karibu nami musikie jambo hili: Tangu mwanzo mimi sikusema kwa siri, tangu mambo hayo yaanze kutendeka, nimekuwa pale. Sasa, Bwana wetu Yawe amenituma, na kunipa nguvu ya Roho wake.


mataifa mengi yataufikia na kusema: Tuende juu kwenye mulima wa Yawe, tuende katika nyumba ya Mungu wa Yakobo, kusudi atufundishe njia zake, nasi tuzifuate. Maana sheria itatoka kule Sayuni; na neno la Yawe kule Yerusalema.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.


Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Mukimbie kutoka Babeli! Mutoke inje ya ile inchi ya Wakaldea, mukuwe kama mabeberu mbele ya kundi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite