Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 2:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yawe anasema hivi: Mukimbie kutoka katika inchi ya kaskazini ambako mimi nilikuwa nimewatawanya kila upande.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 2:10
41 Referans Kwoze  

Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Neno alifanywa kuwa mutu, naye akaishi kati yetu, akijaa neema na ukweli. Tuliona utukufu wake, utukufu ule Mwana wa pekee aliopewa na Baba.


Mushangilie sana enyi watu wa Sayuni! Mupige vigelegele, enyi watu wa Yerusalema! Angalia, mufalme wenu anawakujia, anakuja kwa shangwe na ushindi! Ni mupole, amepanda juu ya punda, juu ya mwana-punda, mutoto wa punda.


Yawe, Mungu wako, yuko pamoja nawe. Yeye ni shujaa anayekuletea ushindi. Yeye atakufurahia kwa furaha kubwa. Kwa upendo wake atakujalia uzima mupya. Atakufurahia kwa wimbo wa sauti kubwa,


Nitaishi kati yao; nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wangu.


Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu nanyi mutakuwa watu wangu.


Nikasikia sauti kubwa tokea kwenye kiti cha kifalme ikisema: “Sasa makao ya Mungu yanapatikana kati ya watu! Yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, naye atakuwa Mungu wao.


Yesu akamujibu: “Anayenipenda, atashika maneno yangu. Baba yangu atamupenda, naye Baba pamoja nami tutaingia ndani yake na kukaa ndani yake.


sauti za arusi na za furaha, sauti za waimbaji wakati wanaleta sadaka za shukrani katika nyumba ya Yawe. Wataimba hivi: Mumushukuru Yawe wa majeshi kwa sababu Yawe ni muzuri, kwa maana wema wake unadumu milele. Nitairudishia inchi hii hali yake ya zamani. –Ni Yawe anayesema.


Humo mutasikilika nyimbo za shukrani nayo makelele ya wenye kufanya sherehe. Nitawaongeza wala hawatakuwa wachache; nitawafanya waheshimiwe wala hawatazarauliwa.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


“Umwandikie malaika wa kanisa la Efeso hivi: “Ujumbe huu unatoka kwa yule anayeshika nyota saba katika mukono wake wa kuume na anayetembea katikati ya vinara saba vya taa vya zahabu.


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


Ninyi mutakimbia kupitia bonde lile, katikati ya milima miwili ya Yawe. Mutakimbia kama vile babu zenu walivyokimbia tetemeko la inchi wakati wa utawala wa mufalme Uzia wa Yuda. Kisha Yawe, Mungu wangu, atakuja na watakatifu wote pamoja naye.


Watakuja na kuimba kwa sauti juu ya mulima Sayuni, watapata utukufu juu ya wema wangu mimi Yawe, kwa ajili ya ngano, divai na mafuta ninavyowapa, kwa ajili ya kondoo na ngombe vilevile; maisha yao yatakuwa kama bustani iliyotiliwa maji, wala hawataregea tena.


Nitafurahi sana kwa sababu ya Yawe, nafsi yangu itashangilia kwa sababu ya Mungu wangu. Maana amenivalisha nguo ya wokovu, amenifunika kanzu ya haki, kama bwana arusi anavyojipamba kwa shada la maua, kama bibi arusi anavyojipamba kwa ushanga wake.


Yawe anasema hivi: Imba kwa shangwe, ewe unayekuwa tasa, wewe ambaye haujapata kuzaa! Piga kelele na kuimba kwa nguvu, wewe usiyepata kuzaa mutoto. Maana watoto wako wewe uliyeachwa watakuwa wengi kuliko wa yule anayekuwa na mume.


Mumwimbie Yawe wimbo mupya! Dunia yote iimbe sifa zake: bahari na vyote vinavyokuwa ndani yake, inchi za mbali na wakaaji wake;


Bwana anakuja kwenye pahali pake patakatifu kutoka Sinai, akikuwa na kundi kubwa, na maelfu na maelfu ya magari ya kukokotwa.


Wewe hautaki sadaka za kuteketezwa kwa moto wala matoleo, sadaka za nyama za kuteketezwa wala za kusamehewa zambi, lakini umenipa masikio nikusikie.


Waliokombolewa na Yawe watarudi, watakuja Sayuni wakipiga vigelegele. Watakuwa wenye furaha ya milele, watajaliwa furaha na shangwe; huzuni na kilio vitatoweka kabisa.


Nitaishi kati ya Waisraeli, nami nitakuwa Mungu wao.


basi huu ndio ujumbe wa Yawe juu ya huyo mufalme: Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa, Watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.


Jumla ya urefu wa kuta zote ine utakuwa ni metre elfu kenda. Jina la muji kutokea sasa na kuendelea litakuwa: Yawe Yupo Hapa.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.


Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.


Haraka! Ninyi wote munaokaa katika inchi ya Babeli, mukimbilie Sayuni!


Yawe atawatawanya kati ya mataifa yote, kutoka pembe moja ya dunia mpaka nyingine na huko mutaitumikia miungu mingine ya miti na mawe, miungu ambayo ninyi wala wazee wenu hamukuijua.


Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite