Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 14:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wakati ule hakutakuwa baridi wala baridi kali.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 14:6
24 Referans Kwoze  

Kisha malaika wa saba akapiga baragumu. Halafu sauti kubwa zikasikilika katika mbingu, zikisema: “Sasa utawala juu ya dunia ni wa Bwana wetu na wa Masiya wake. Naye atatawala kwa milele na milele!”


Vilevile tunaamini ujumbe uliotangazwa na manabii. Ninyi munafanya vema mukishikamana nao. Ujumbe huo ni kama taa inayoangaza pahali pa giza, mpaka wakati wa mapambazuko na wakati nyota ya asubui itakapoangazia mioyo yenu.


Mimi nimekuja katika dunia kama mwangaza, kusudi mutu yeyote anayeniamini asikae katika giza.


Mutu wa usawa anaangaziwa mwangaza katika giza; yeye ni mwenye huruma, rehema, na haki.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


mumushukuru Mungu Baba aliyewawezesha ninyi kuwa wenye kustahili kupokea sehemu yenu ya urizi aliowawekea watu wake katika ufalme wa mwangaza.


Mwangaza ule uliangaza katika giza, wala giza halikuuzimisha.


Basi tumutambue, tujikaze sana kumujua Yawe. Kuja kwake ni hakika kama mapambazuko, yeye atatufikia kama vile manyunyu, kama vile mvua za kwanza zinavyolowanisha udongo.


Niliangalia dunia, nikaona imekuwa ukiwa na tupu; niliangalia mbingu, nazo hazikukuwa na mwangaza.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza; jua linapochomoza litakuwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake.


Lakini jambo hili ni lile lililosemwa na nabii Yoeli.


Nami nitafanya maajabu juu katika mbingu na vitambulisho chini katika dunia: kutakuwa damu, moto na moshi mwingi.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Nitakapokuangamiza, nitazifunika mbingu, nitazifanya nyota kuwa nyeusi, jua nitalifunika kwa mawingu, na mwezi hautatoa mwangaza wake.


Nitaifanya miangaza yote mbinguni kuwa giza nitatandaza giza juu ya inchi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Hiyo ni siku ya giza na huzuni; siku ya mawingu na giza nene. Jeshi kubwa linakaribia kama giza linalofunikia milima. Namna hiyo haijapata kuwa hata kidogo wala haitaonekana tena katika vizazi vyote vinavyokuja.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite