Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 14:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 14:3
22 Referans Kwoze  

Siku hiyo, nitayaangamiza mataifa yote yanayotaka kuushambulia Yerusalema.


Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza. Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa na kubadilisha haya yao kuwa sifa na utukufu katika dunia yote.


Hata juu ya watumishi wanaume na wanawake, nitashusha Roho wangu wakati huo.


Yahazieli akasema: “Musikilize ninyi watu wa Yuda na wakajii wa Yerusalema na mufalme Yosafati, Yawe anawaambia hivi: musiogope wala musihangaike kwa sababu ya jeshi hili kubwa. Vita hivi si vyenu, lakini ni vya Mungu.


Aliweza kuitwaa inchi hii yote kwa sababu Yawe, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.


Naye Yawe akawatia hofu kubwa mbele ya Waisraeli ambao waliwaua watu wengi kule Gibeoni wakiwakimbia kwenye njia ya muteremuko wa Beti-Horoni mpaka Azeka na Makeda ambako vilevile waliwaua watu wengi sana.


Hakujakuwa siku kama hiyo hata kidogo wala haijapata kuonekana tena, siku ambayo Yawe amemwitikia mwanadamu kwa namna hiyo; maana Yawe mwenyewe aliwapigania Waisraeli.


Ukiwa pahali popote unapofanya kazi, mara utakaposikia baragumu, kimbilia kwetu. Mungu wetu atatupigania.”


Halafu, kundi la mataifa yote yanayoshambulia Yerusalema, wote wanaoshambulia ukuta wake na kuutia wasiwasi, watatoweka kama ndoto, kama maono ya usiku.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite