Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 14:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Lakini juu ya wale watu ambao walikuja kupigana na Yerusalema, hizi ndizo hasara ambazo Yawe atawaletea: Miili yao itaoza wangali wazima; macho yao yataoza yakiwa kwenye matundu yake na ndimi zao zitaoza zikiwa katika vinywa vyao.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 14:12
34 Referans Kwoze  

Siku hiyo, nitayaangamiza mataifa yote yanayotaka kuushambulia Yerusalema.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayeona matokeo ya kasirani yako?


Wewe mwenyewe utapata ugonjwa mukali wa tumbo, ambao utaongezeka siku kwa siku, mpaka matumbotumbo yako yatoke inje.”


basi, Yawe atawaletea ninyi na wazao wenu mateso yasiyokuwa ya kawaida, mateso makali yasiyoponyeshwa na ya kudumu, na magonjwa makali ya kudumu.


Yawe atawashambulia kwa kifua kikuu, homa, majipu, joto kali, ukavu, zoruba na ukungu; mambo hayo yatawaandama mpaka muangamie.


basi nami nitapingana nanyi kwa hasira kali, na kuwaazibu mimi mwenyewe mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


basi, nami nitapingana nanyi na kuwaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Kama mukiendelea kunipinga na kukataa kunisikiliza, nitazidisha tena azabu yenu mara saba kadiri ya wingi wa zambi zenu.


basi, mimi nitafanya hivi: Nitawapiga kwa kuwaletea hofu kubwa ya rafla, kifua kikubwa na homa itakayowapofusha macho na kuwakondesha. Mutapanda mbegu zenu bila mafanikio maana waadui zenu ndio watakaozikula.


Zile pembe kumi ulizoona na yule nyama wa ajabu watamuchukia yule kahaba. Watamunyanganya vyote anavyokuwa navyo na kumwacha uchi. Nao watakula nyama ya mwili wake na kuteketeza mabaki yake kwa moto.


Na pale pale malaika wa Bwana akamwazibu Herode kwa ugonjwa kwa sababu alijitukuza kwa pahali pa Mungu. Herode akakuliwa na michango ya tumbo na kisha akakufa.


Na kama hata kisha kuazibiwa hivyo hamutanisikiliza, basi, nitawaazibu mara saba zaidi kwa ajili ya zambi zenu.


Atawaletea ugonjwa mukali mpaka ninyi wote muangamie kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi.


Ugonjwa mukali unakula ngozi yake, ugonjwa wa kifo unaharibu viungo vyake.


Hasara kubwa zitapata farasi, nyumbu, ngamia, punda na nyama wote watakaokuwa katika kambi zile za waadui.


Ikiwa Wamisri watakataa kushiriki kwa sikukuu ya Vibanda, basi, Yawe atawapiga kwa ugonjwa uleule atakaowapiga nao mataifa yote yanayokataa kushiriki kwa sikukuu hiyo.


Lakini nimekasirikia sana mataifa ambayo yanastarehe. Nilikuwa ninayakasirikia kidogo, lakini yaliwaongezea hasara.


Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite