Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 14:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Inchi yote, tangu Geba mpaka Rimoni, upande wa kusini wa Yerusalema, itageuzwa kuwa mbuga yenye kunyooka kabisa. Lakini Yerusalema utabaki juu pahali pake tokea mulango wa Benjamina mpaka kwenye mulango wa zamani, hata kwenye mulango wa Konani, tangu munara wa Hanameli mpaka kwenye kikamulio cha mufalme.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 14:10
28 Referans Kwoze  

Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.


Alipokuwa katika mulango wa Benjamina, mulinzi mumoja anayeitwa Iria mwana wa Selemia, mujukuu wa Hanania, alimukamata Yeremia na kumwambia: Wewe unatoroka kusudi uende kujiunga na Wakaldea!


Yawe anasema hivi: Nitatengeneza upya maisha ya jamaa za wazao wa Yakobo, nitayaonea makao yao huruma; muji wao utajengwa upya kwenye mabomoko yake, nyumba ya kifalme itasimama pahali ilipokuwa mbele.


Halafu mufalme Asa akatoa tangazo kwa watu wote wa Yuda, bila kumwacha hata mutu mumoja, wahamishe mawe ya Rama na mbao, vifaa ambavyo Basha alivitumia kwa kujenga. Kisha mufalme Asa alitumia vifaa hivyo kwa kujenga kuta za Geba, katika inchi ya Benjamina na Misipa.


Nami nikauliza: Watu hawa wanakuja kufanya nini? Yeye akanijibu: Watu hawa wamekuja kuyatisha na kuyaangamiza yale mataifa yenye nguvu ambayo yaliishambulia inchi ya Yuda na kuwatawanya watu wake.


Lakini Ebedimeleki, towashi Mwetiopia aliyetumika katika nyumba ya kifalme, alipata habari kwamba walikuwa wamemutia Yeremia katika kisima. Wakati huo mufalme alikuwa anafanya baraza kwenye mulango wa Benjamina.


Basi Eliasubu, Kuhani Mukubwa, pamoja na wandugu zake waliokuwa makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango wa kondoo. Wakautakasa na kutia milango yake; wakaitakasa tangia kwenye Munara wa Mia Moja mpaka Munara wa Hananeli.


Lakini wanaume mia sita wa kabila la Benjamina walipata kukimbilia katika jangwa mpaka kwenye mulima wa Rimoni, wakakaa kule kwa muda wa miezi mine.


Watu wengine wa kabila la Benjamina wakakimbia kuelekea upande wa jangwa mpaka kwenye mulima wa Rimoni. Wengine elfu tano waliuawa kwenye njia kubwa walipokuwa wanakimbia. Waisraeli waliendelea kuwafuatilia vikali watu wa kabila la Benjamina mpaka kwenye muji wa Gidomu, wakawaua watu elfu mbili.


Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.


Amekwisha pita kwenye kivuko. Usiku huu analala Geba. Watu wa Rama wanatetemeka kwa hofu, wakaaji wa Gibea, muji wa Sauli, wamekimbia.


Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,


Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.


Halafu Yoasi mufalme wa Israeli alimukamata Amazia mufalme wa Yuda, mwana wa Yoasi, mwana wa Ahazia kule Beti-Semesi akamupeleka mpaka Yerusalema. Kule, akabomoa ukuta wa muji ule, kuanzia kwenye mulango wa Efuraimu mpaka kwenye mulango wa Pembeni, umbali wa karibu metre mia mbili.


Kisha wote pamoja wakawapelekea ujumbe wa amani watu wa kabila la Benjamina ambao walikuwa kwenye mulima wa Rimoni.


Katika eneo la kabila la Benjamina walipewa miji mingine: Gibeoni pamoja na mbuga zake za malisho,


Yoasi mufalme wa Israeli alimuteka Amazia mufalme wa Yuda mwana wa Yoasi mwana wa Ahazia kule Beti-Semesi. Halafu akauendea Yerusalema na kuubomoa ukuta wake kutoka kwenye Mulango wa Efuraimu mpaka kwenye Mulango wa Pembeni, umbali wa karibu metre mia mbili.


Basi, Pashuri akamupiga nabii Yeremia na kumutia katika minyororo iliyokuwa upande wa mulango wa juu wa kuingilia katika nyumba ya Yawe, ulioitwa mulango wa Benjamina.


Tena Uzia akajenga minara ya kukinga muji kwenye milango tatu ya Yerusalema na kuiimarisha.


Kutakuja wakati ambapo mulima wa nyumba ya Yawe utakuwa mukubwa kuliko milima yote. Utanyanyuliwa juu ya vilima vyote. Watu wengi watakimbilia kule,


Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite