Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 13:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 13:9
54 Referans Kwoze  

Uniite wakati wa taabu, nami nitakuokoa, nawe utanitukuza.”


Halafu watu wote watakaoomba kwa jina la Bwana ataokolewa.’


Mimi nimekusafisha lakini si kama feza katika furu. Nimewapima katika furu ya taabu.


Akiniita, mimi nitamwitikia; akikuwa katika taabu nitakuwa pamoja naye, nitamwokoa na kumupa heshima.


Yule atakayeshinda atapokea toka kwangu zawadi ile, mimi nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwana wangu.


Wandugu wapendwa, musishangae kwa kuona mateso makubwa ya kuwajaribu munayopata. Musiyahesabu kuwa kitu kigeni kwenu.


Mutakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.


Mukipita katika maji, mimi nitakuwa pamoja nanyi; mukipita katika mito, haitawashinda nguvu. Mukitembea katika moto, hamutaungua; ulimi wa moto hautawaunguza.


Heri mutu yule anayevumilia wakati anapojaribiwa, kwa maana akiisha kushinda majaribu, atapokea ile taji ya uzima ambayo Mungu aliahidia wale wanaomupenda.


Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.


Sasa hili ndilo agano nitakalofanya na watu wa ufalme wa Israeli katika siku zile: nitawawezesha kuchunga sheria zangu ndani ya mafikiri yao, nikiziandika ndani ya mioyo yao. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo. Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.


Lakini yeye anajua njia ninayofuata; atakapomaliza kunipima nitatoka mule safi kama zahabu.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Kisha siku hizo, nitafanya agano hili na Waisraeli. Nitaiweka sheria yangu ndani yao, na kuiandika katika mioyo yao. Mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Halafu mutaomba, nami Yawe nitawaitikia; mutalia kwa sauti kwa kuomba musaada, nami nitajibu hivi: Niko hapa! Kama mukiondoa mambo ya kitumwa, mukiacha kuzarau wengine na kusema maovu,


Nitatembea kati yenu na kuwa Mungu wenu nanyi mutakuwa watu wangu.


Halafu nitawajaza wazao wa Daudi na wakaaji wa muji Yerusalema roho ya huruma na maombi, nao watamwangalia yule waliyemutoboa kwa mukuki; watamulilia kama vile mutu anavyolia kwa kifo cha mutoto wake wa pekee, au kama vile mutu anavyomulilia kwa uchungu muzaliwa wake wa kwanza.


Zahabu na feza vinapimwa kwa moto, lakini Yawe ndiye anayepima mioyo ya watu.


Heri taifa ambalo limejaliwa hayo! Heri taifa ambalo Yawe ndiye Mungu wao!


Nitaishi kati yao; nitakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wangu.


Mutakaa katika inchi niliyopatia wazee wenu. Mutakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu.


kusudi mupate kufuata masharti yangu na kuyatii maagizo yangu; nanyi mutakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wenu.


Nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao.


Malaika wa kwanza akapiga baragumu. Halafu mvua ya mawe na moto vyenye kuchanganyika na damu, vikatupwa katika dunia. Sehemu moja ya tatu ya inchi ikateketea, na sehemu moja ya tatu ya miti na majani yote vikateketea vilevile.


Kisha malaika wa pili akapiga baragumu. Halafu kitu kimoja chenye kufanana na mulima mukubwa unaowaka moto kikatupwa katika bahari, na sehemu moja ya tatu ya bahari ikageuka damu.


Sehemu moja ya tatu ya viumbe vinavyoishi katika bahari vikakufa, na sehemu moja ya tatu ya mashua ikaharibika.


Kisha malaika wa tatu akapiga baragumu. Halafu nyota kubwa iliyowaka kama mwenge, ikaanguka toka mbinguni na kujitupa juu ya sehemu moja ya tatu ya mito na juu ya chemichemi.


(Jina la ile nyota ni Uchungu.) Basi sehemu moja ya tatu ya maji ikakuwa uchungu, na watu wengi waliokunywa maji yale walikufa kwa sababu ya sumu iliyokuwa ndani yake.


Kisha malaika wa ine akapiga baragumu. Sehemu moja ya tatu ya jua ikaharibishwa pamoja na sehemu moja ya tatu ya mwezi na ya nyota. Sehemu zile tatu zikaingiwa na giza. Hivi hakukuwa mwangaza kwa muda wa sehemu moja ya tatu ya saa za muchana na sehemu moja ya tatu ya saa za usiku vilevile.


Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama tini hizi zinavyokuwa nzuri, ndivyo nitakavyowaona kuwa wema watu wa Yuda ambao niliowaondoa toka nafasi hii na kuwapeleka katika uhamisho katika inchi ya Wababeli.


Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Wamoja kati ya wenye hekima watauawa, kusudi wapate kuondolewa uchafu, kutakaswa na kusafishwa, mpaka wakati wa mwisho, ambao sasa bado haujatimia.


Watu wengi wataondolewa uchafu, watatakaswa na kusafishwa. Lakini watu waovu wataendelea kutenda uovu. Hakuna hata mumoja wa hao waovu atakayeelewa; wenye hekima ndio watakaoelewa.


Hata umewaimarisha watu wako Waisraeli kwa ajili yako mwenyewe, kusudi wakuwe watu wako milele; nawe ee Yawe umekuwa Mungu wao.


Hakika kuna nafasi ya kuchimba feza, na pahali ambako zahabu inasafishwa.


Hapo, ee Mungu, nitakwenda kwenye mazabahu yako; nitakuja kwako, ee Mungu, wewe furaha yangu kubwa. Nitakusifu kwa zeze, ee Mungu, Mungu wangu.


Mupenzi wangu ni wangu, nami ni wake. Yeye anakulisha kondoo wake penye yungiyungi.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitawasafisha na kuwapima kwa moto kama vile chuma. Ni namna gani zaidi ya kuwatendea hawa watu wangu waovu?


Kwa hiyo Waisraeli hawataniacha tena na kujichafua wenyewe kwa kutenda zambi; kusudi wakuwe watu wangu nami nikuwe Mungu wao. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite