Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 13:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 13:2
40 Referans Kwoze  

Yawe akamwuliza: ‘Kwa namna gani?’ Naye akajibu: ‘Nitakwenda na kuwasukuma manabii wake wote waseme uongo.’ Yawe akamwambia: ‘Wewe utamushawishi na utashinda; basi, kwenda ufanye hivyo.’


Huko nitamurudishia mashamba yake ya mizabibu. Bonde la Akori litakuwa mulango wa tumaini. Ataniitikia vizuri kama vile alipokuwa kijana, kama wakati alipotoka katika inchi ya Misri.


Ushike mambo yote niliyokuambia. Usiyataje hata kidogo majina ya miungu mingine, hayo yasisikilike katika kinywa chako.


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitaharibu sanamu za miungu, na kukomesha miungu ya uongo ya muji wa Nofi. Hakutakuwa mukubwa tena huko Misri. Nitasababisha hofu itawale katika inchi ya Misri.


Yule nyama akakamatwa pamoja na yule nabii wa uongo aliyeonyesha vitambulisho mbele yake. (Ni kwa njia ya vitambulisho vile aliwadanganya wale waliopigwa chapa ya yule nyama na wale walioabudu sanamu yake.) Nyama yule pamoja na nabii wa uongo wakatupwa wangali wazima katika ziwa la moto munamowaka mawe ya kiberiti.


Kwa ngambo yangu, ikiwa mimi ninafukuza pepo kwa uwezo wa Mungu, hii inaonyesha kwamba Ufalme wa Mungu umekwisha kufika kati yenu.


“Wakati pepo imekwisha kutoka ndani ya mutu, inazungukazunguka katika jangwa kutafuta nafasi ya kupumzikia. Naye asipopata nafasi ile,


Wao watamwogopa sana Yawe; ataiangamiza miungu yote ya dunia. Mataifa yote katika dunia yatamwabudu; kila taifa katika pahali pake.


Kama mutu angetokea akitangaza maneno matupu ya uongo na kusema “Ninawatabiria divai na pombe kwa wingi”, muhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!


Hawatajichafua tena kwa kuabudu sanamu za miungu yao na kwa mambo yao ya kuchukiza wala kwa makosa yao. Nitawaokoa wasikuwe tena waasi. Nao watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.


Na ikiwa nabii yule akidanganyika na kusema kitu, basi mimi Yawe nimemupotosha. Nami nitanyoosha mukono wangu kwa kumwondoa nabii yule kutoka kwa watu wangu Waisraeli.


basi, ninyi hamutapata tena maono madanganyifu, wala hamutatabiri tena. Nitawaokoa watu wangu toka katika mikono yenu. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Jambo hili litawafikia kwa sababu wametenda katika Israeli mambo yasiyofanyika. Walizini na wake za jirani zao, na kusema maneno ya uongo kwa jina langu, jambo ambalo mimi sikuwaamuru wafanye. Mimi ninajua hayo. Nimeyashuhudia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo sanamu za feza na zahabu walizojitengenezea kusudi waziabudu.


Sanamu zote za miungu zitatoweka kabisa.


Lakini wanaoabudu miungu mingine, watapata mateso mengi. Sitaitolea sadaka za damu hata kidogo, na majina ya miungu hiyo sitayataja.


Musishirikiane na mataifa haya yaliyobaki kati yenu. Musiitaje miungu yao wala musiape kwa majina ya miungu yao; musiitumikie wala kuinama mbele yao.


Muvunje mazabahu zao, na kubomoa kabisa nguzo zao. Muteketeze kwa moto sanamu zao za Ashera na kukatakata sanamu zao za kuchonga na kufuta kabisa jina lao na pahali hapo.


Mutu akiazima nyama kwa mwenzake, kisha nyama yule akaumia au akakufa wakati mwenye naye hayuko, aliyeazima nyama yule anapaswa kumulipa kwa ukamilifu.


Halafu akalalamika kwa sauti kubwa, akisema: “Umebomoka, umebomoka kabisa ule muji mukubwa Babeli! Sasa umekuwa makao ya mashetani ya kila namna, ya pepo wachafu, na makimbilio ya ndege wote wachafu na wenye kuchukiza.


“Mufanye angalisho na manabii wa uongo; kwa maana wanakuja kwenu wakionekana kwa inje kama vile kondoo, lakini ndani, wao ni kama imbwa wakali wa pori.


Watarudi na kuishi chini ya ulinzi wangu, watastawi kama bustani nzuri. Watachanua kama muzabibu, harufu yao nzuri kama ya divai ya Lebanoni.


Pahali pote munapoishi, miji yenu itakuwa ukiwa na sehemu zenu zinazoinuka za kutambikia zitabomolewa, mazabahu zenu zitabomolewa na kuwa ukiwa, sanamu zenu za miungu zitavunjwa na kuharibiwa. Pahali penu pa kufukizia ubani patabomolewa na chochote mulichofanya kitatoweka.


Maana hakutakuwa tena maono ya uongo au uaguzi kati ya Waisraeli.


Nitawaokoa kutoka uchafu wenu wote. Nitaiamuru ngano iongezeke, wala sitawaletea njaa tena.


Lakini nabii yeyote atakayesema kwa jina la miungu mingine, au atakayejaribu kusema neno kwa jina langu wakati mimi sikumwambia aseme, huyo nabii atakufa.’


naye akaniambia: Wewe mwanadamu! Hapa ndipo pahali pa kiti changu cha kifalme, pahali ninapoweka miguu yangu. Nitakaa kati ya watu wa Israeli milele. Na Waisraeli hawatalichafua jina langu, wao wenyewe, wala wafalme wao kwa kuziabudu sanamu au kuzika maiti za wafalme wao pahali hapa.


Maana, nitalifanya jina la Bali lisitajike tena katika kinywa chako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite