Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 13:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 13:1
34 Referans Kwoze  

Na wamoja kati yenu walikuwa kama wao. Lakini mumesafishwa toka zambi, mumetakaswa na kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa jina la Bwana Yesu Kristo na kwa Roho wa Mungu wetu.


Kesho yake Yoane akamwona Yesu akikuja kwake, akasema: “Angalia Mwana-Kondoo wa Mungu anayeondoa zambi ya dunia!


Nitawanyunyizia maji safi, nanyi mutakuwa safi. Nitawatakasa toka uchafu wenu wote na toka uchafu wa sanamu za miungu yenu yote.


Yesu Kristo ndiye aliyekuja kwa maji ya ubatizo wake na kwa damu ya kufa kwake. Hakukuja na maji tu, lakini pamoja na maji na damu. Naye Roho ndiye anayeshuhudia mambo yale kwa sababu Roho ni wa ukweli.


Lakini kama tunaishi katika mwangaza kama vile Mungu mwenyewe anavyokaa katika mwangaza, tunashirikiana sisi kwa sisi, na damu ya Mwana wake Yesu inasafisha zambi zetu zote.


Ee Yawe, tumaini la Waisraeli, wote wanaokukataa wafezeheshwe. Wanaokuacha wewe watatoweka, kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi, kwa maana wamekuacha wewe Yawe, unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.


Lakini mulikombolewa kwa njia ya damu yenye bei kali ya Kristo, aliyekuwa kama kondoo asiyekuwa na kilema wala uchafu.


Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.


Mimi ni mukosaji tangia kuzaliwa kwangu, mwenye zambi tangia tumbo la mama yangu.


Nitawaokoa kutoka uchafu wenu wote. Nitaiamuru ngano iongezeke, wala sitawaletea njaa tena.


Wewe mwanadamu! Waisraeli walipoishi katika inchi yao waliichafua kwa mienendo na matendo yao. Niliyaona matendo yao kuwa sawa na mwanamuke anayekuwa muchafu wakati wa ugonjwa wake wa mwezi.


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.


Yawe amekufanya wewe Zefania kuwa kuhani kwa pahali pa kuhani Yehoyada, kusudi ukuwe mukubwa wa nyumba ya Yawe. Wewe utashugulika na kumutia katika kifungo na kumufunga kwa minyororo mwenda-wazimu yeyote anayetabiri.


Nitatakasa zambi zao zote na kuwasamehe uovu wao na uasi walionitendea.


Yule mutu akanirudisha kwenye kiingilio cha hekalu. Huko, maji yalikuwa yakitoka chini ya kizingiti cha hekalu kuelekea upande wa mashariki, (kwa maana hekalu lilielekea upande wa mashariki). Maji yalikuwa yakitiririka kutoka chini ya upande wa kusini wa mulango wa hekalu, upande wa kusini wa mazabahu.


Jamaa zote zilizobaki zitaomboleza: wanaume peke yao na wanawake peke yao.


Hata hivyo, kisima au chemichemi ya maji vitakuwa safi. Lakini kitu chochote kinachogusa muzoga kitakuwa kichafu.


Mutachota maji kwa furaha kutoka visima vya wokovu.


Nitaziharibu sanamu zenu, na nguzo zenu za ibada; nanyi mutakoma kuabudu vitu mulivyotengeneza wenyewe.


kwa sababu malaika wa Bwana alishuka mara kwa mara ndani ya kile kisima na kutikisa maji. Na mugonjwa wa kwanza aliyeingia ndani ya maji kisha kuyatikisa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite