Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:8
53 Referans Kwoze  

Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.


Katika maono mengine, nilimwona mutu aliyekuwa na kamba ya kupima katika mukono wake.


Nao watu wa mataifa watakapoona hayo, watafezeheka hata kama wana nguvu. Watapigwa na bumbuazi na kukosa cha kusema na kuwa kama viziwi.


Usifurahie hali yangu ewe adui yangu! Nikianguka, nitasimama tena; nikiwa katika giza, Yawe ni mwangaza wangu.


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


“Mimi Yesu, nimemutuma malaika wangu kwa kuwashuhudia maneno haya yote katika kanisa. Mimi ni wa shina na wa uzao wa mufalme Daudi. Mimi ni nyota ya asubui.”


Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho.”


walizimisha moto mukali, waliponyoka kuuawa kwa upanga. Walikuwa wazaifu, lakini wakapata nguvu; walikuwa shujaa katika vita na kushinda majeshi ya kigeni.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Wao ni wazao wa babu zetu, na Kristo alizaliwa kimwili katika kizazi chao. Yeye ndiye mukubwa kupita wote na Mungu anayesifiwa kwa milele! Amina.


“Angalia bikira atapata mimba, atazaa mutoto mwanaume, naye ataitwa Emanueli,” (maana yake “Mungu yuko pamoja nasi”).


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Yawe ana mashitaki juu ya Yuda; atawaazibu wazao wa Yakobo kadiri ya makosa yao, na kuwalipa kadiri ya matendo yao.


Hao wanawatabiria uongo. Jambo hilo litawasababisha ninyi kuhamishwa mbali na inchi yenu. Nitawafukuza mbali, nanyi mutaangamia.


Katika taabu zao zote, hakumutuma mujumbe mwingine kwa kuwasaidia, lakini yeye mwenyewe alikuja kuwaokoa; kwa upendo na huruma yake aliwakomboa. Aliwabeba na kuwakamata tangu zamani.


Alizarauliwa na kukataliwa na watu. Alikuwa mutu wa uchungu na huzuni. Alikuwa kama mutu wa kuchukiza kwa watu; alizarauliwa na tukamwona si kitu.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Mimi nilisema kwamba ninyi ni miungu, kwamba ninyi wote ni wana wa Mungu Mukubwa!


Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.


Basi, malaika wa Mungu aliyekuwa mbele ya kundi la Waisraeli akaondoka akakaa nyuma yao. Na ule munara wa wingu vilevile ukaondoka mbele ukasimama nyuma yao.


Nitamutuma malaika awaongoze. Nitawafukuza Wakanana, Waamori, Wahiti, Waperizi, Wahivi na Wayebusi.


Watano wenu watafukuza waadui mia moja na mia moja wenu watafukuza waadui elfu kumi. Waadui zenu wataangamia mbele yenu kwa upanga.


Mutu wenu mumoja tu anaweza kuwakimbiza waadui elfu moja, maana Yawe Mungu wenu ndiye anayewapigania kama alivyowaahidi.


mutu ni nini, ee Mungu, hata umufikirie? Mwanadamu ni nini hata umujali?


Yawe aliniambia hivi: Simba mukali ananguruma kwa kukinga nyama aliyemukamata; hata kundi la wachungaji likiitwa kwa kumufukuza, hatishiki kwa kelele zao, wala hashituki kwa sauti zao. Ni vile Yawe wa majeshi atakavyoshuka kupigana juu ya mulima Sayuni na kilima chake.


Yawe atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana wetu Yawe atapiga baragumu; atafika pamoja na upepo mukali wa kusini.


Hakuna atakayesema tena ni mugonjwa; watu watasamehewa uovu wao wote.


Watu wa Efuraimu watakuwa kama mashujaa katika vita; watajaa furaha kama watu waliokunywa divai. Watoto wao wataona hayo na kufurahi, watajaa furaha ndani ya moyo kwa sababu yangu mimi Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite