Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Nami Yawe nitasaidia kwanza jamaa za Yuda kusudi wazao wa Daudi na wakaaji wa Yerusalema wasijione kuwa wenye utukufu zaidi kuliko watu wengine wa kabila la Yuda.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:7
20 Referans Kwoze  

Yawe anasema hivi: Nitatengeneza upya maisha ya jamaa za wazao wa Yakobo, nitayaonea makao yao huruma; muji wao utajengwa upya kwenye mabomoko yake, nyumba ya kifalme itasimama pahali ilipokuwa mbele.


Basi sasa mutu ataweza kujivuna? Hapana! Kwa sababu gani? Kwa sababu anatii Sheria? Hapana. Lakini kwa sababu anamwamini Yesu.


Na agano hilo likavunjwa siku ileile. Wale wachuuzi wa kondoo waliokuwa wananiangalia, wakajua kwamba neno la Yawe lilikuwa limenifikia.


Yule malaika akaniambia vilevile niseme neno hili la Yawe juu ya Zerubabeli: Hauwezi kushinda kwa nguvu au kwa uwezo wako mwenyewe, lakini kwa musaada wa roho wangu. –Ni Yawe wa majeshi anayesema.


Siku inakuja nitakapoisimika nyumba ya Daudi iliyoanguka; nitazitengeneza kuta zake, na kusimika upya mabomoko yake. Nitaijenga upya kama ilivyokuwa tangu zamani.


Ni Yawe wa majeshi! Yeye ndiye aliyeyapanga haya yote. Alifanya hivyo akiharibu kiburi chao na kuwapatisha haya waheshimiwa wake.


Uharibifu umeenea popote katika muji, maovu na mapotovu kila pahali.


Lakini ninakutumainia wewe, ee Yawe; wewe, ee Yawe, Mungu wangu, ndiwe utakayenijibu.


Uwaache hao wanaofurahia hasara yangu, washindwe wote na kufezeheka. Hao wote wanaojiona bora kuliko mimi, wapate haya na kufezeheka.


Munaishusha hali yangu mupate kujipandisha; munanitusi kwa kunyenyekezwa kwangu.


Lakini Mungu ametujalia neema kubwa zaidi, kwa maana Maandiko yanasema: “Mungu anapingana na wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”


Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.


Saa ile ile, Yesu akajazwa na furaha kwa uwezo wa Roho Mutakatifu, naye akasema: “Ee Baba, Bwana wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo. Ndiyo Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite