Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Siku hiyo, ninasema mimi Yawe, nitamutia hofu kila farasi, na askari mupanda-farasi wake nitamufanya kuwa mwenda-wazimu. Farasi wa mataifa mengine nitawapofusha. Lakini kabila la Yuda nitalilinda.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:4
24 Referans Kwoze  

Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.


Yawe atawapiga kwa pigo la kuwa na wazimu, mutakuwa vipofu na kuvurugika akili.


Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.


Mungu hahesabu tena nyakati zile watu walipokuwa katika ujinga, lakini sasa anatangaza kwa watu wote, na nafasi zote kwamba wageuke toka zambi zao.


Hasara kubwa zitapata farasi, nyumbu, ngamia, punda na nyama wote watakaokuwa katika kambi zile za waadui.


Siku hiyo kutakuwa maombolezo makubwa katika Yerusalema kama vile maombolezo ya kumwomboleza Hadadi-Rimoni katika bonde la Megido.


Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.


Mimi mwenyewe nitailinda inchi yangu, nitazuia majeshi yasipitepite ndani. Hakuna mutu atakayewatesa tena watu wangu, maana, kwa macho yangu mwenyewe, nimeona jinsi walivyoteseka.


Tega sikio, ee Mungu wangu; angalia uone taabu tunazokuwa nazo na jinsi huo muji unaoitwa kwa jina lako unavyotaabika. Tunakutolea maombi yetu si kwa sababu tumetenda haki, lakini kwa sababu wewe una huruma nyingi.


Kwenye meza yangu, watashibishwa kwa farasi, waaskari wapanda-farasi, mashujaa na watu wote wa vita. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Mimi nitakugeuza na kukutia ndoana katika mataya yako, na kukutoa inje wewe pamoja na kundi lako lote la waaskari: farasi na waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa la watu wanaovaa nguo za vita, ngao kubwa na ndogo katika mikono pamoja na mapanga yao.


Nitawalinda siku zote na kuwarudisha katika inchi hii. Nitawajenga, wala sitawabomoa; nitawapanda, wala sitawaongoa.


Ee, Yawe, fungua macho uone, tega sikio lako uyasikie matusi yote ambayo Saniharibu amepeleka na kukutukana wewe Mungu Mwenye Uzima.


Siku ile Yawe ataliazibu jeshi la anga vilevile na wafalme wa dunia.


Usikilize kwa uangalifu maombi yangu, na uniangalie mimi mutumishi wako, ninapokuomba kwa ajili ya watumishi wako, watu wa Israeli, usiku na muchana. Ninaungama zambi za watu wa Israeli, tulizofanya mbele yako. Mimi pamoja na watu wa jamaa yangu tumefanya zambi.


Sasa nitachunga hekalu hili na kusikiliza maombi yatakayofanyika hapa,


“Sasa ee Mungu wangu, utuangalie na upokee maombi tutakayoomba pahali hapa.


Uchunge nyumba hii muchana na usiku pahali ambapo umechagua watu wako waliabudie jina lako. Unisikilize mimi mutumishi wako ninapokuja pahali hapa kuomba.


Waaramu waliposhambulia, Elisha alimwomba Yawe akisema: “Ninakuomba ufanye watu hawa wakuwe vipofu!” Yawe akasikiliza ombi lake na kuwafanya vipofu.


Kwa hiyo mufalme akatuma kule kundi kubwa la waaskari pamoja na farasi na magari ya vita. Kundi hilo likafika kule wakati wa usiku na kuuzunguka muji.


Uchunge nyumba hii usiku na muchana, nafasi ambapo umesema: ‘Hapo ndipo watu watakapoliheshimu jina langu’. Unisikilize ninapokuja pahali hapa kwa kuomba.


Kwa hiyo wakubwa wa Yuda wataambiana: “Wakaaji wa Yerusalema wamepata nguvu yao kutoka kwa Yawe wa majeshi, Mungu wao.”


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite