Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Siku hiyo nitaufanya Yerusalema kuwa kama jiwe zito kwa watu wote: yeyote atakayelinyanyua atajiumiza mwenyewe. Watu wa mataifa yote katika dunia wataushambulia muji ule.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:3
31 Referans Kwoze  

Anayeanguka juu ya jiwe hili atavunjikavunjika, na yule litakayemwangukia, atapondekana.]”


Kila mutu atakayeanguka juu ya jiwe lile, atavunjika na yule litakayemwangukia, litamuponda.”


Wakati ule hakutakuwa baridi wala baridi kali.


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Siku hiyo kutakuwa maombolezo makubwa katika Yerusalema kama vile maombolezo ya kumwomboleza Hadadi-Rimoni katika bonde la Megido.


Hawa ndio pepo wanaoonyesha vitambulisho. Nao ndio wanaokwenda kwa wafalme wote wa dunia na kuwakusanya kwa kupigana vita Siku ile kubwa ya Mungu Mwenye Uwezo.


Siku ile, hofu kutoka kwa Yawe itawapata watu, na kila mutu atamushambulia mwenzake.


Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.


Siku hiyo, ninasema mimi Yawe, nitamutia hofu kila farasi, na askari mupanda-farasi wake nitamufanya kuwa mwenda-wazimu. Farasi wa mataifa mengine nitawapofusha. Lakini kabila la Yuda nitalilinda.


na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.


Wakati huo, nitawaazibu wote wanaokugandamiza. Nitawaokoa vilema na kuwakusanya waliotupwa na kubadilisha haya yao kuwa sifa na utukufu katika dunia yote.


Mateso uliyoyatenda kule Lebanoni yatakulemea wewe; uliwaua nyama, nyama nao watakuogopesha. Yote hayo yatakupata wewe, kwa mauaji na mateso uliyoitendea dunia, uliyoifanyia miji na wakaaji wake wote.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Wazao wa Yakobo watakuwa kama moto na wazao wa Yosefu kama ndimi za moto. Watawaangamiza wazao wa Esau kama vile moto unavyoteketeza majani yenye kukauka, hakutaponyoka hata mumoja wao. –Yawe amesema.


Kila ufalme au taifa lisilokutumikia litaangamizwa; mataifa hayo yatateketezwa kabisa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite