Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Nitaufanya Yerusalema kuwa kama kikombe cha divai; na mataifa yanayokuwa kandokando yake yatakunywa na kuyumbayumba kama walevi. Muji Yerusalema utakaposhambuliwa, hata miji yote ya Yuda itashambuliwa.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:2
15 Referans Kwoze  

Watu wa Yuda watapigana kwa kuulinda Yerusalema; utajiri wa mataifa yote yanayoizunguka inchi ya Yuda utakusanywa: watakusanya zahabu, feza na nguo kwa wingi sana.


Mungu mwenyewe ndiye mwamuzi; anamushusha mumoja na kumwinua mwingine.


Amuka, ewe Yerusalema! Amuka usimame wima! Yawe amekukunywesha kikombe cha kasirani yake, nawe umekikunywa mpaka tone la mwisho, mpaka ukayumbayumba.


Mutendee muji ule sawa vile ulivyowatendea. Mulipize matendo yake mara mbili zaidi. Na katika kile kikombe alimochanganya divai yake, mumuchangie divai inayokuwa kali mara mbili zaidi kuliko ile aliyowapa.


Na ule muji mukubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, na miji ya mataifa yote ikabomoka. Mungu hakusahau muji mukubwa Babeli, akaukunywesha kikombe kinachokuwa na divai ya kasirani yake kali.


naye vilevile atakunywa divai kali ya hasira ya Mungu iliyotengenezwa pasipo kuchangwa na maji na kumimiwa ndani ya kikombe chenye kujaa kasirani yake! Na watu kama wale, watateswa ndani ya moto na ndani ya mawe ya kiberiti yanayowaka moto mbele ya wamalaika watakatifu na mbele ya Mwana- Kondoo.


Utajaa haya pahali pa heshima. Utakunywa wewe mwenyewe na kupepesuka! Yawe mwenyewe atakulewesha, na haya itaifunika heshima yako!


Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!


Babeli ilikuwa kikombe cha zahabu katika mukono wa Yawe, ambacho kiliilewesha dunia nzima. Mataifa yalikunywa divai yake; kwa hiyo, yakapata wazimu.


Yawe anasema hivi: Ikiwa wale ambao hawakustahili kunywa kikombe cha azabu ni lazima wakikunywe, basi, wewe utaachwa bila kuazibiwa? Hapana! Hautakosa kuazibiwa; ni lazima ukunywe hicho kikombe!


Basi, nikatwaa kikombe hicho toka mukono wa Yawe, nikayakunywesha mataifa yote ambayo Yawe alinituma kwao.


Yawe, Mungu wa Israeli, akaniambia hivi: Twaa toka katika mukono wangu kikombe hiki cha divai kinachojaa kasirani yangu uyakunyweshe mataifa yote ninayokutuma kwao.


Watu wanauliza: Kwa nini sisi tunakaa tu hapa? Tukusanyike, tuingie katika miji yenye kuzungukwa na kuta, tuangamie kule! Yawe, Mungu wetu, amekusudia tuangamie, ametupa maji yenye sumu tukunywe, kwa sababu tumemukosea yeye.


Yawe atayakusanya mataifa yote kwa kuushambulia Yerusalema. Muji utakamatwa, nyumba zenu zitatekwa, na wanawake wenu watakamatwa kwa kinguvu. Nusu ya wakaaji wa muji watapelekwa katika uhamisho, lakini nusu itakayobaki haitaondoshwa inje ya muji.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite