Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 ukoo wa Lawi peke yake na ukoo wa Simei peke yake.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:13
16 Referans Kwoze  

Wana wengine wane wa Simei walikuwa: Yahati, Zina, Yeusi na Beria.


Wana wa Gersoni walikuwa: Ladani na Simei.


Simei alikuwa na wana kumi na sita na wabinti sita, lakini wandugu zake hawakukuwa na wana wengi, na jamaa yake vilevile haikuongezeka kama kabila la Yuda. Miji walimokuwa wakiishi mpaka wakati wa utawala wa mufalme Daudi ilikuwa: Beri-Seba, Molada, Hasari-Suali, Biliha, Ezemi, Toladi, Betueli, Horma, Ziklagi, Beti-Makaboti, Hasari-Susimu, Beti-Biri na Sarayimu, Etamu, Aini, Rimoni, Tokeni na Asani, pamoja na vijiji kandokando ya miji hiyo mpaka Bali. Hayo ndiyo yaliyokuwa makao yao, nao wakaandika majina yao katika vitabu vya vizazi vyao.


Wana wa Pedaya walikuwa: Zerubabeli na Simei. Wana wa Zerubabeli walikuwa: Mesulamu na Hanania. Alikuwa na binti mumoja, jina lake Selomiti.


Lakini kuhani Zadoki, Benaya mwana wa Yehoyada, nabii Natani na Simei, na Rei pamoja na walinzi wa Daudi, hawakumwunga Adonia mukono.


Wakati Daudi alipofika kule Bahurimu, kulitokea mutu mumoja wa ukoo wa Saulo, jina lake Simei mwana wa Gera, akaanza kumulaani Daudi kwa mufululizo.


Inchi itaomboleza, kila ukoo utaomboleza peke yake: wanaume peke yao na wanawake peke yao, ukoo wa Daudi peke yake, ukoo wa Natani peke yake,


Jamaa zote zilizobaki zitaomboleza: wanaume peke yao na wanawake peke yao.


Na haya ndiyo majina ya wana wa Gersoni kwa kufuata jamaa zao: Libuni na Simei.


Wana wa Kohati kwa kufuata jamaa zao: Amuramu, Isihari, Hebroni na Uzieli.


Wana wa Merari kwa kufuata jamaa zao: Mali na Musi. Hizi zilikuwa jamaa za Walawi kulingana na ukoo zao.


Jamaa za Walibuni na Wasimei zilitokana na Gersoni; hizi ndizo zilizokuwa jamaa za Wagersoni.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite