Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 12:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Inchi itaomboleza, kila ukoo utaomboleza peke yake: wanaume peke yao na wanawake peke yao, ukoo wa Daudi peke yake, ukoo wa Natani peke yake,

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 12:12
17 Referans Kwoze  

Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


Kisha kitambulisho cha kurudi kwa Mwana wa Mutu kitaonekana katika mbingu. Nayo mataifa yote ya dunia yatakuwa katika malalamiko, na yatamwona Mwana wa Mutu akikuja katikati ya mawingu toka mbinguni, kwa uwezo na utukufu mukubwa.


na kuwauliza makuhani wa hekalu la Yawe wa majeshi maneno haya: Tuendelee kuomboleza na kufunga kula chakula katika mwezi wa tano kama tulivyofanya kwa muda wa miaka mingi sasa?


Haya ndiyo majina ya wana ambao wake zake walimuzalia kule Yerusalema: Samua, Sobabu, Natani, Solomono,


Musinyimane, isipokuwa tu mumepatana na kwa muda tu kusudi mupate wakati wa kujitoa kwa kufunga na kuomba. Kisha munaweza kurudiliana tena kusudi Shetani asiwajaribu katika uzaifu wenu.


Muwakusanye watu wote, muwatakase watu. Muwalete wazee, muwakusanye watoto, hata watoto wanaonyonya. Bwana-arusi na bibi-arusi watoke katika vyumba vyao.


Nimesikia Efuraimu akilalamika hivi: Umeniazibu vikali, maana nilikuwa kama mwana-ngombe asiyezoea nira. Unigeuze nami nitakugeukia, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wangu.


Muambie mufalme na malkia mama yake hivi: Mushuke toka kwenye viti vyenu vya kifalme, maana taji zenu nzuri zimeanguka toka juu ya vichwa vyenu.


Kwa hiyo, inchi itaomboleza, na mbingu zitakuwa nyeusi. Maana nimesema nami sitabadilisha nia yangu; nimeamua, wala sitarudi nyuma.


Kelele linasikilika juu ya vilima: Waisraeli wanalia na kuomboleza, kwa sababu wamepotoka katika njia zao, wamenisahau mimi Yawe, Mungu wao.


Basi Yawe akamutuma nabii Natani kwa Daudi. Natani alimwendea Daudi, akamwambia: “Kulikuwa wanaume wawili katika muji mumoja. Mumoja alikuwa tajiri na mwingine alikuwa masikini.


Basi mufalme, watumishi wake na wakaaji wote wa Misri wakaamuka usiku. Kukakuwa kilio kikubwa katika inchi yote ya Misri kwa maana hakukuwa hata nyumba moja ambamo mutu hakukufa.


Siku hiyo kutakuwa maombolezo makubwa katika Yerusalema kama vile maombolezo ya kumwomboleza Hadadi-Rimoni katika bonde la Megido.


ukoo wa Lawi peke yake na ukoo wa Simei peke yake.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite