Basi watumishi wake walipomutoa katika gari lake la vita, wakamubeba na gari lake la pili mpaka Yerusalema. Naye akakufa na kuzikwa katika makaburi ya kifalme. Watu wote wa inchi ya Yuda na Yerusalema wakaomboleza kifo cha Yosia.
Wakati wa kutawala kwake, Neko mufalme wa Misri alikwenda mpaka kwenye muto Furati kwa kukutana na mufalme wa Asuria. Naye mufalme Yosia akaondoka kwa kupigana naye; lakini Neko mufalme wa Misri alipomwona akamwua kule Megido.
Kisha kitambulisho cha kurudi kwa Mwana wa Mutu kitaonekana katika mbingu. Nayo mataifa yote ya dunia yatakuwa katika malalamiko, na yatamwona Mwana wa Mutu akikuja katikati ya mawingu toka mbinguni, kwa uwezo na utukufu mukubwa.
Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.
Lakini Yosia hakukubali kumwachilia. Akakataa kusikiliza maneno Mungu aliyosema kwa njia ya Neko, kwa hiyo akajibadilisha kusudi asitambulikane, kisha akaingia katika vita katika bonde la Megido.