Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 11:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 11:8
25 Referans Kwoze  

“Kama dunia ikiwachukia ninyi, mujue kwamba ilinichukia mimi mbele ya kuwachukia.


Watu wa dunia hawawezi kuwachukia ninyi, lakini wananichukia mimi kwa sababu ninashuhudia kwamba matendo yao ni mabaya.


Yawe, Mukombozi na Mutakatifu wa Israeli, anamwambia hivi yule anayezarauliwa sana, yule anayechukiwa na mataifa, na ambaye ni mutumishi wa watawala: Wafalme wataona nao watasimama; wakubwa watainama na kuabudu kwa heshima ya Yawe ambaye anatimiza ahadi zake, kwa heshima ya Mutakatifu wa Israeli ambaye amekuchagua wewe.


Lakini wanainchi wenzake walimuchukia. Kwa hiyo wakatuma wajumbe kumufuata nyuma waende kusema: ‘Hatutaki mutu huyu kuwa mufalme wetu.’


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Mwenye haki mbele yangu ataishi kwa njia ya imani. Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”


Yawe anasema hivi: Uovu wao wote ulianzia Gilgali; kule ndiko nilipoanza kuwachukia. Kwa sababu ya uovu wa matendo yao, nitawafukuza toka katika nyumba yangu. Sitawapenda tena. Wakubwa wao wote ni waasi.


Usitutupe, kwa ajili ya heshima ya jina lako; usikizarau kiti chako cha kifalme chenye utukufu. Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.


Wachaguliwa wangu wamenigeuka, wamekuwa kama simba katika pori, wameningurumia mimi; ndiyo maana ninawachukia.


Hasira ya Yawe ikawawakia watu wake, akachukizwa sana na hao waliokuwa mali yake.


Yawe aliona jambo hilo akawaacha; aliwakataa watoto wake, wanaume na wanawake.


Lakini, kwa hayo yote, wanapokuwa katika inchi ya waadui zao, mimi sitawatupa wala kuwachukia hata kuwaangamiza kabisa na kuvunja agano langu.


Nitaharibu pahali penu pa ibada kule juu ya milima, nitabomoa mazabahu zenu za kufukizia ubani, na kutupa maiti zenu juu ya sanamu za miungu yenu. Roho yangu itawachukia kabisa.


Nitaweka makao yangu kati yenu, wala sitawaachilia.


Niko na muzigo wa mateso ninaopaswa kubeba, nami ninasongwa sana mpaka mapaswa hayo yatakapotimizwa!


Watu wa Efuraimu, pinde na mishale katika mukono, walirudi nyuma, wakakimbia siku ile ya vita.


Wewe si Mungu anayependa ubaya; mwovu hawezi kupokelewa kwako.


Basi wataitwa “takataka za feza”, maana mimi Yawe nimewakataa.


Mimi Yawe nitaigusa mioyo ya Waisraeli kusudi wanirudilie, maana wamejitenga mbali nami kwa kuabudu sanamu zao za miungu.


Kweli wewe ni mutoto wa mama aliyemuchukia mume wake na watoto wake; wewe ni sawa na dada zako waliowachukia waume wao na watoto wao. Mama yako alikuwa Muhiti na baba yako alikuwa Mwamori.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Resoni alikuwa adui wa Waisraeli siku zote za utawala wa Solomono, akamusumbua sana Solomono kama naye Hadadi alivyomusumbua. Basi, Resoni aliizarau inchi ya Israeli, naye alitawala inchi ya Aramu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite