Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 11:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kisha nikawaambia: Kama mukipendezwa, munilipe mushahara wangu; lakini kama munaona sivyo, basi muache. Basi, wakanipimia vikoroti makumi tatu vya feza kwa mushahara wangu.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 11:12
16 Referans Kwoze  

na kuwaambia: “Mutanipa nini kama nikimutoa Yesu kwenu?” Basi wakamupa vikoroti makumi tatu vya feza.


Kama ngombe yule akimupiga pembe mutumwa au mujakazi, mwenye ngombe atamulipa bwana wa yule mutumwa feza zenye bei ya shekeli makumi tatu na yule ngombe anapaswa kuuawa kwa kupigwa mawe.


Wachuuzi Wamidiani walipofika pahali pale, wale wandugu wakamwondoa Yosefu katika shimo, wakamwuzisha kwa Waisimaeli kwa bei ya vikoroti makumi mbili vya feza; nao wakamupeleka Yosefu Misri.


Wakati Yesu na wanafunzi wake walipokuwa wakikula chakula cha magaribi, Shetani alikuwa amekwisha kumushawishi Yuda mwana wa Simoni Iskariota kwamba amutoe Yesu.


Basi, siku moja, Ahabu akamwambia Naboti: “Unipe shamba lako la mizabibu nilifanye shamba la mboga, kwa sababu liko karibu na nyumba yangu. Nitakupa shamba lingine zuri zaidi, au ukitaka nitakulipa feza sawasawa na bei yake.”


Mupango huu ukamupendeza mufalme pamoja na watu wote waliokuwa wamekusanyika.


Halafu yakatimia maneno yaliyosemwa na nabii Yeremia: “Walitwaa vikoroti makumi tatu vya feza kufuatana na bei Waisraeli waliyoipanga juu yake,


wakazitumia kwa kununua shamba la Mufinyanzi, sawa vile Bwana alivyoniamuru.”


Abrahamu akakubaliana na Efuroni, akamupimia kadiri ya feza alizotaja mbele ya Wahiti wote, feza vikoroti mia ine, kadiri ya vipimo vya wachuuzi wa wakati ule.


Solomono alikuwa na vibanda elfu makumi ine kwa ajili ya farasi wa magari yake ya kukokotwa, na waaskari wapanda-farasi elfu kumi na mbili.


Nikalinunua shamba hilo linalokuwa kule Anatoti, kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nikamulipa bei yake vikoroti kumi na saba vya feza.


Yawe wa majeshi anasema: Kisha nitawakaribia kwa kuwahukumu. Sitasita kutoa ushuhuda juu ya wachawi, wazinzi, watoa ushuhuda wa uongo, wanaopunja mushahara wa watumishi, wanaowatesa wajane na wayatima, wanaozuia mugeni asipate haki yake na wale wasioniogopa mimi.


Kama ni mwanamuke, atakombolewa kwa feza shekeli makumi tatu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite