Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 11:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Na agano hilo likavunjwa siku ileile. Wale wachuuzi wa kondoo waliokuwa wananiangalia, wakajua kwamba neno la Yawe lilikuwa limenifikia.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 11:11
27 Referans Kwoze  

Nitakuachia watu wapole na wanyenyekevu ambao watakimbilia usalama kwangu mimi Yawe.


Lakini hawakupata namna ya kumwua, kwa sababu watu wote walimusikiliza kwa uangalifu.


Halafu Yesu akawajibu wale wajumbe: “Mwende kumwelezea Yoane mambo muliyoona na kusikia: vipofu wanapata kuona, viwete wanatembea, wenye ukoma wanatakaswa, viziwi wanapata kusikia, wafu wanafufuliwa na Habari Njema inahubiriwa kwa wamasikini.


Basi, akafika saa ile ile, akaanza kumushukuru Mungu. Naye akaeleza habari za mutoto huyo kwa watu wote waliokuwa wakingojea jinsi Mungu atakavyokomboa Yerusalema.


Wakati ule katika Yerusalema kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Simeoni. Mutu huyo alikuwa mwenye haki na mwenye kuogopa Mungu. Alikuwa akitazamia kwa hamu ukombozi wa taifa la Israeli. Roho Mutakatifu alikuwa pamoja naye;


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Lakini wote wanaomutumainia Yawe, watapata nguvu mupya. Watapanda juu kwa mabawa kama tai, watakimbia bila kuchoka, watatembea bila kuregea.


Basi watapewa jibu gani wajumbe wa taifa hilo? Wataambiwa: Yawe ameijenga imara Sayuni, na wamasikini kati ya watu wake watakimbilia kule.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Wanyenyekevu wataona hayo na kufurahi; wanaomutafuta Mungu watapata moyo.


Maana ninajua kwamba nyuma ya kifo changu hakika mutakuwa waovu na kuacha ile njia niliyowaamuru muifuate. Na katika siku zinazokuja mutapatwa na hasara kwa sababu mutafanya maovu mbele ya Yawe na kumukasirikisha kwa matendo yenu.”


Watakapopatwa na hasara nyingi na taabu, wimbo huu utakuwa kama ushuhuda maana hautasahauliwa na wazao wao. Hata sasa, mbele sijawapeleka katika inchi niliyoapa kuwapa, ninajua mipango ambayo wanapanga.”


zaidi ya zahabu aliyopokea kutoka kwa wafanya biashara na wachuuzi, tena kutoka kwa wafalme wote wa Arabia na watawala wa inchi ya Israeli.


Kisha binamu yangu Hanameli akanifikia katika baraza la walinzi kama alivyonifahamisha Yawe, akaniambia: Nunua shamba langu linalokuwa kule Anatoti katika inchi ya Benjamina maana wewe uko na haki ya kulikomboa. Ulinunue kwa faida yako. Basi nikajua kwamba neno hili ni la Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite