Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.
Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–
Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.
Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.
Kutokana na makosa yenu, mutataabika kwa muda wa miaka makumi ine, sawa na zile siku makumi ine mulizopeleleza ile inchi, mwaka mumoja kwa kila siku moja; mutatambua kwamba mimi nimechukizwa.