Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 11:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Nikakamata ile fimbo yangu niliyoiita “Rehema”, nikaivunja, kuonyesha kwamba agano Yawe alilofanya na watu wake limevunjwa.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 11:10
20 Referans Kwoze  

Basi, nikakuwa muchungaji wa kondoo ambao wachuuzi waliwatayarisha kwenda kuchinjwa. Nikatwaa fimbo mbili: moja nikaiita “Rehema”, na ingine nikaiita “Umoja”, nikaenda kuchunga kondoo.


Lakini sasa, ee Mungu, umemutupa na kumukataa, umejaa kasirani juu ya huyo uliyemuchagua.


Usitutupe, kwa ajili ya heshima ya jina lako; usikizarau kiti chako cha kifalme chenye utukufu. Ukumbuke agano ulilofanya nasi, wala usilivunje.


“Kweli ninawaambia: hiki kizazi hakitapita mbele ya kutimia kwa mambo yote.


Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Si wangu”, maana ninyi si watu wangu, wala mimi si Mungu wenu.


Utuonyeshe uzuri wako, ee Bwana, Mungu wetu; uimarishe kazi zetu, uziimarishe.


Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kisha majuma hayo makumi saba na mawili, yule aliyepakwa mafuta atauawa na hatabaki na kitu. Muji na Pahali Patakatifu Sana vitaharibishwa na waaskari wa mutawala atakayekuja kushambulia. Mwisho wake utafika kama mafuriko, kukiwa vita na maangamizi kama yalivyopangwa na Mungu.


Uwaambie Waisraeli kwamba: Bwana wetu Yawe anasema hivi: Nitalichafua hekalu langu, hiyo nyumba ambayo munajivunia na kuitegemea na ambao munafurahi sana kuiona.


Kutoka Sayuni, muji muzuri kupita kipimo, Mungu anajitokeza, akiangaza.


Kutokana na makosa yenu, mutataabika kwa muda wa miaka makumi ine, sawa na zile siku makumi ine mulizopeleleza ile inchi, mwaka mumoja kwa kila siku moja; mutatambua kwamba mimi nimechukizwa.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite