Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Japo niliwatawanya kati ya mataifa, hata hivyo, watanikumbuka wakiwa humo. Nao pamoja na watoto wao wataishi na kurudi katika nyumba zao.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:9
24 Referans Kwoze  

Halafu wale walioponyoka watanikumbuka katikati ya mataifa ambamo watakuwa wamepelekwa katika uhamisho. Nitakuwa nimewavunja moyo wao wa uzinzi ambao ulinitupilia mbali, na macho yao yaliyozini na sanamu zao. Kwa hiyo watajichukia wao wenyewe kwa sababu ya maovu na machukizo yao yote waliyoyatenda.


Wazao wa Yakobo watakaobaki wazima, wataenea kati ya mataifa na watu wengi watakuwa na nguvu kubwa kama simba kati ya nyama wa pori, kama simba mukali kati ya makundi ya kondoo, ambaye kila pahali anapopita, anarukia na kurarua nyama, na hakuna mutu yeyote wa kuiokoa.


Siku hiyo, nitajibu kwa mahitaji ya mbingu ya kunyesha mvua, mbingu nazo zitajibu kwa mahitaji ya udongo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Siku zinakuja ambapo nitaijaza inchi ya Israeli na inchi ya Yuda watu na nyama kama vile mulimaji anavyopanda mbegu.


Kazi zao hazitakuwa bure, wala hawatazaa watoto watakaopatwa na musiba; maana watakuwa waliobarikiwa na Yawe, wamebarikiwa wao pamoja na wazao wao.


Nitawajalia watu wa Yakobo, na Yuda nitamujalia watakaorizi milima yangu; wachaguliwa wangu watairizi, watumishi wangu watakaa kule.


Katika kila jimbo na kila muji, popote pale tangazo hili liliposomwa, Wayuda wakafurahi na kushangilia, wakafanya sherehe na mapumziko; na watu wengine wengi wakajifanya kuwa Wayuda, maana waliwaogopa sana Wayuda.


Lakini mukinirudilia, mukishika amri zangu na kuzifuata hata ingawa nitakuwa nimewatawanya mbali kabisa, nitawarudisha pahali nilipochagua kuwa pahali pangu pa kuabudiwa.’


Ninyi mulioponyoka kifo, muondoke sasa, wala musisitesite! Ingawa muko katika inchi ya mbali, mumukumbuke Yawe, muukumbuke vilevile Yerusalema.


Nitatoa amri, na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifa kama mutu anavyopepeta ngano kusudi niwatoshe wote wasiofaa.


Ninyi watu wa mataifa mengine ni kama tawi la muzeituni wa pori lililokatwa na kisha likapandikizwa ndani ya muzeituni uliopandwa, umbalimbali na kawaida. Wayuda ni kama muzeituni huu uliopandwa; na si neno gumu basi kwa Mungu kupandikiza tena matawi yaliyokatwa katika muti wao wenyewe.


Wale waamini waliosambaa walikwenda popote wakitangaza Habari Njema.


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


Yawe anasema hivi: Ewe Israeli, watu wa Yakobo, kumbuka kwamba wewe ni mutumishi wangu. Nilikuumba kusudi ukuwe mutumishi wangu, nami sitakusahau hata kidogo.


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite