Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Nitawaita watu wangu na kuwakusanya pamoja; nimekusudia kuwakomboa, nao watakuwa wengi kama vile mbele.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:8
25 Referans Kwoze  

Yawe ananyunyua bendera kwa kuita taifa la mbali; anawapigia filimbi watu kutoka miisho ya dunia; nao wanakuja mbio na kufika haraka!


Wakati huo, Yawe atawapigia muunzi watu wa Misri wakuje kama mainzi toka vijito vya mito Nili; na watu wa Asuria wakuje kama nyuki kutoka inchi yao.


Kama vile nyota katika anga na muchanga katika bahari visivyoweza kuhesabiwa, ndivyo nitakavyoongeza hesabu ya wazao wa mutumishi wangu Daudi na hesabu ya makuhani wa ukoo wa Lawi.


Roho na Bibi arusi wanasema: “Kuja!” Naye mwenye kusikia maneno haya aseme vilevile: “Kuja!” Yule anayesikia kiu akuje, na yule anayetaka maji ya uzima akuje kuyapokea kwa bure.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya agano langu pamoja nanyi, agano lililokamilishwa kwa njia ya damu, nitawakomboa wafungwa wenu wanaokuwa kama wamefungwa katika shimo tupu.


Watu wako uliowakomboa, ee Yawe, watarudia, watakuja Sayuni wakiimba; watajaa furaha ya milele, watapata furaha na shangwe. Huzuni na maombolezo vitatoweka kabisa.


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Watu wa Yuda na wa Israeli walikuwa wengi kama muchanga wa bahari, nao walikuwa wakikula, wakikunywa, na kufurahi.


Lakini wazao wa Israeli wakaongezeka sana, wakakuwa wengi na wenye nguvu sana, wakaenea kila pahali katika inchi ya Misri.


Kisha mambo haya, nikaangalia nami nikaona mukutano mukubwa sana wa watu wasioweza kuhesabiwa. Kulikuwa watu wa kila taifa, wa kila kabila, wa kila jamaa na wa kila luga. Walikuwa wakisimama mbele ya kiti cha kifalme na mbele ya Mwana-Kondoo, wakivaa kanzu nyeupe na kushika matawi ya muti wa ngazi katika mikono yao.


Watakuja makundi kwa makundi na kuyajaza mabonde yenye miinuko, mapango ndani ya mawe, miiba, vichaka vyote na mashamba yote ya kukulishia nyama.


Sasa, muondoke Babeli! Mukimbie kutoka kwa Wakaldea! Mutangaze jambo hili kwa sauti za shangwe. Mueneze habari zake kila pahali katika dunia. Museme: Yawe amekomboa taifa la mutumishi wake Yakobo.


Lakini kweli nitawakusanya ninyi wote enyi watu wa Yakobo, nitawakusanya enyi Waisraeli muliobaki, niwalete pamoja kama kondoo katika zizi, kama kundi kubwa la kondoo katika shamba la malisho; nanyi mutakuwa kundi la watu wengi.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite