Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Watu wa Efuraimu watakuwa kama mashujaa katika vita; watajaa furaha kama watu waliokunywa divai. Watoto wao wataona hayo na kufurahi, watajaa furaha ndani ya moyo kwa sababu yangu mimi Yawe.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:7
31 Referans Kwoze  

Yawe wa majeshi atawalinda watu wake, nao watawaangamiza waadui zao. Watapiga kelele katika vita kama walevi, wataimwanga damu ya waadui zao. Itatiririka kama damu ya nyama wanaotolewa kwa sadaka iliyomiminwa juu ya mazabahu kutoka ndani ya bakuli.


Ninyi munamupenda ijapokuwa hamujamwona, na munamwamini ijapokuwa sasa hamumwoni. Na zaidi ya ile munashangilia kwa furaha isiyoweza kuelezwa, inayojaa utukufu,


Mufurahi siku zote katika kuungana kwenu na Bwana. Na tena ninasema: Mufurahi!


Ni kwa hiyo moyo wangu unafurahi, ulimi wangu unashangilia, nami ninakaa na matumaini,


Na sasa ninyi vilevile munasikia uchungu, lakini nitawaona tena, nanyi mutafurahi, wala hakuna mutu atakayeweza kuwahuzunisha tena.


roho yangu inamufurahia Mungu, Mwokozi wangu;


Angalia jinsi gani uzuri na urembo wake unavyokuwa! Vijana wanaume na wanawake watastawi kwa wingi wa ngano na divai mupya.


Imba kwa sauti, ewe Sayuni, piga vigelegele, ee Israeli. Furahi na kushangilia kwa moyo wote, ewe Yerusalema!


mimi nitaendelea kumufurahia Yawe. Nitamushangilia Mungu anayeniokoa.


Nitawapa moyo mumoja na nia moja, wapate kuniheshimu mimi siku zote, kwa faida yao wenyewe na kwa faida ya watoto wao watakaofuata.


Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.


Wanaokuwa wazima ndio wanaokushukuru, kama na mimi ninavyofanya leo. Wababa wanajulisha watoto wao uaminifu wako.


apate divai ya kumuchangamusha, mafuta ya muzeituni ya kumwangarisha, na mukate wa kumupa nguvu.


Lakini wewe unabaki sawasawa, na maisha yako hayana mwisho.


Yawe ndiye nguvu na ngao yangu; tegemeo la moyo wangu ni kwake. Amenisaidia, nami nikashangilia kwa moyo wote; kwa wimbo wangu ninamushukuru.


Usiwaache waadui zangu waseme: “Tumemushinda huyu!” Watesaji wangu wasifurahie kuanguka kwangu.


Halafu Hana aliomba na kusema: Ninamushangilia Yawe ndani ya moyo wangu. Ninamutukuza Yawe anayekuwa nguvu yangu. Ninawachekelea waadui zangu; maana ninaufurahia wokovu wako.


Chakula kilikuwa kikitwaliwa kutoka kwenye meza ya Yosefu na kupelekwa kwao, lakini Benjamina alipewa mara tano zaidi ya kipimo wandugu zake walichopewa. Basi, wakakunywa na kufurahi pamoja naye.


Nimemuchagua yeye na wazao wake. Yeye atawafundisha wazao wake kushika njia yangu kwa kutenda kwa haki na kwa kufuata sheria yangu, nami nitawatimizia ahadi zangu.”


ameitimiza kwa ajili yetu sisi wazao wao. Amefanya hivi kwa kumufufua Yesu kwa kuhakikisha maandiko haya ya Zaburi ya pili yanayosema: ‘Wewe ni mwana wangu, mimi leo ninakuwa baba yako.’


Kwa maana ahadi hii ya Mungu ilitolewa kwenu, kwa watoto wenu na kwa wote wanaokaa mbali, ndio wote ambao Bwana Mungu wetu atakaowaita.”


Utuonyeshe matendo yako sisi watumishi wako; uwaonyeshe wazao wetu utukufu wako.


Tunafurahi kwa sababu yake; tunatumainia jina lake takatifu.


Watu wako watafundishwa nami Yawe, wana wako watapata ustawi mwingi.


Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.


Mufurahi, enyi watu wa Sayuni, mushangilie kwa sababu ya Yawe, Mungu wenu, maana amewapa mvua zinazowafalia, amewapa mvua ya kutosha: mvua za kwanza na mvua za katikati kama pale mbele.


Siku ile, watu wote watasema: Huyu ndiye Mungu wetu! Tumemungojea atuokoe. Huyu ndiye Yawe tuliyemutazamia. Mukuje tufurahi na kushangilia kwa sababu ametuokoa.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite