Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nitawaimarisha watu wa Yuda; nitawaokoa wazao wa Yosefu. Nitawarudisha kwao kwa maana ninawaonea huruma, nao watakuwa kama vile sikuwa nimewakataa. Mimi ni Yawe, Mungu wao, nami nitayasikiliza maombi yao.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:6
39 Referans Kwoze  

Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Mimi nitawaimarisha watu wangu, nao watanitii na kuishi kwa kunipendeza. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Siku hizo, watu wa Yuda wataungana na watu wa Israeli, na wote kwa pamoja watatoka katika inchi ya kaskazini na kurudi katika inchi niliyowapa babu zenu ikuwe urizi wao.


Lakini sasa sitawatendea hao watu wa taifa hili wanaobaki kama vile zamani. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.–


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Waisraeli wataniomba niwafanye kuwa wengi kama kundi la kondoo, nami nitawafanya hivyo.


Basi, usiogope, mimi nipo pamoja nawe. Usifazaike, mimi ni Mungu wako. Nitakuimarisha na kukusaidia; nitakulinda kwa mukono wangu wa ushindi.


Nao watu wa mataifa watakapoona hayo, watafezeheka hata kama wana nguvu. Watapigwa na bumbuazi na kukosa cha kusema na kuwa kama viziwi.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


Yawe anasema: Enyi watu wa Sayuni, musimame muwakanyagekanyage! Nitawapatia nguvu kama ngombe dume mwenye pembe za chuma na kwato za shaba. Mutawasaga watu wa mataifa mengi; mutanitolea mimi mapato yao, mutanitolea mali zao mimi Bwana wa dunia yote.


Siku hiyo, nitajibu kwa mahitaji ya mbingu ya kunyesha mvua, mbingu nazo zitajibu kwa mahitaji ya udongo. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yawe atawahurumia tena watu wa Yakobo, atawachagua tena Waisraeli. Atawarudisha katika inchi yao wenyewe, na wageni watakuja na kukaa pamoja na watu wa Yakobo.


Kwa hiyo Bwana wetu Yawe anasema hivi: Sasa nitawahurumia Waisraeli wazao wa Yakobo, na kuwarudishia fanaka yao. Ninataka jina langu takatifu liheshimiwe siku zote.


Wewe mwanadamu, twaa kijiti kimoja, uandike juu yake maneno haya: Kwa Yuda na Waisraeli wanaoshirikiana naye. Kisha twaa kijiti kingine uandike juu yake maneno haya: Kwa Yosefu (kijiti cha Efuraimu) na Waisraeli wanaoshirikiana naye.


Nitawafanya watu na nyama waongezeke na kuwa wengi. Nitawafanya ninyi milima mukaliwe tena kama zamani. Nitawatendea mema mengi kuliko zamani. Nanyi mutatambua kwamba mimi ni Yawe.


Siku zinakuja ambapo nitafanya agano jipya na watu wa Israeli na watu wa Yuda.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kutakuja siku ambazo nitakuwa Mungu wa jamaa zote za Waisraeli, nao watakuwa watu wangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Yawe anasema hivi: Nitatengeneza upya maisha ya jamaa za wazao wa Yakobo, nitayaonea makao yao huruma; muji wao utajengwa upya kwenye mabomoko yake, nyumba ya kifalme itasimama pahali ilipokuwa mbele.


Katika siku za utawala wake, inchi ya Yuda itaokolewa na inchi ya Israeli itakuwa katika usalama. Naye ataitwa kwa jina la Yawe Ni Haki Yetu.


Nimemupata mutumishi wangu Daudi; nimemuchagua kwa kumupakaa mafuta yangu matakatifu.


Siku ile, nitawakusanya waliolemewa, nitawakusanya waliopelekwa katika uhamisho, watu wale ambao niliwaazibu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Wazao wa Yakobo watakuwa kama moto na wazao wa Yosefu kama ndimi za moto. Watawaangamiza wazao wa Esau kama vile moto unavyoteketeza majani yenye kukauka, hakutaponyoka hata mumoja wao. –Yawe amesema.


Lakini nitawahurumia watu wa Yuda na kuwaokoa. Mimi Yawe, Mungu wao, nitawaokoa, lakini si kwa nguvu za waaskari, au pinde, au panga, au farasi au waaskari wapanda-farasi.


Naye atasimika bendera kuwaita mataifa, kuwakusanya Waisraeli waliozarauliwa, kuwaleta pamoja watu wa Yuda waliotawanywa, na kuwarudisha toka pembe ine za dunia.


Usiogope, hautapata haya tena. Usifazaike, hautazarauliwa tena. Utaisahau haya uliyopata katika ujana wako, wala hautakumbuka tena mazarau ya ujane wako.


Kwa hasira nyingi nilikuficha uso wangu kwa muda kidogo, lakini kwa wema wa milele nitakuonea huruma. Ni Yawe Mukombozi wako anayesema hivyo.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.


Wakati ule, Yawe, Mungu wao, atawaokoa, maana wao ni kundi lake; nao watangaa katika inchi yake kama mawe ya bei kali katika taji.


Watoto wao watakuwa kama walivyokuwa zamani, nayo makundi yatasimama imara mbele yangu, nami nitawaazibu wote wanaowagandamiza.


Enyi watu wa Efuraimu, muko na maneno gani tena na sanamu? Mimi ndiye ninayesikiliza maombi yenu, mimi ndiye ninayewatunza. Mimi nitawapa kivuli kama cha muti wa muberoshi; kutoka kwangu mutapata matunda yenu.


Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite