Biblia Todo Logo
Bib sou entènèt

- Piblisite -




ZAKARIA 10:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.

Gade chapit la Kopi




ZAKARIA 10:5
40 Referans Kwoze  

na kuangusha falme na kukomesha nguvu zao. Nitayapindua magari yao ya vita na waaskari wapanda-farasi wake, nao wataanguka na kuuana wao kwa wao.


Siku hiyo, mimi Yawe nitawalinda wakaaji wa Yerusalema. Wanaokuwa wazaifu zaidi kati yao watakuwa na nguvu kama mufalme Daudi. Wazao wa Daudi watashika usukani kwa kuwaongoza watu wa Yuda kama Mungu, au kama malaika wa Yawe.


Yuda nitamutumia kama upinde wangu; Efuraimu nimemufanya mushale wangu. Ee Sayuni, watu wako nitawatumia kama upanga kwa kuwashambulia watu wa Ugriki; watakuwa kama upanga wa shujaa.


Ninajua Yawe atamusaidia mufalme aliyemuchagua, atamujibu tokea pahali pake patakatifu mbinguni; kwa mukono wake wenye nguvu atamujalia ushindi mukubwa.


Nimeshindana vizuri, nimekimbia na kufika mwisho wa mashindano yangu. Nimelinda imani yangu.


Silaha tunazotumia katika vita si za kimwili, lakini silaha zetu ni uwezo wa Mungu unaoweza kuharibu upango wa adui. Tunaharibu mawazo ya uongo na


Musa akafundishwa mambo yote ya hekima ya Wamisri, akakuwa mwenye uwezo sana katika masemi yake na matendo yake.


Naye akawauliza: “Ni mambo gani?” Nao wakamujibu: “Haujui mambo yaliyomupata Yesu wa Nazareti? Yeye alishuhudiwa na Mungu na watu wote kwamba alikuwa nabii mwenye uwezo katika mambo aliyofanya na kusema.


Shetani akamufikia na kumwambia: “Kama wewe ni Mwana wa Mungu, amuru mawe haya yageuke kuwa mikate.”


Siku ile, hofu kutoka kwa Yawe itawapata watu, na kila mutu atamushambulia mwenzake.


Kisha Yawe atatoka na kuyapiga vita mataifa hayo, kama vile anavyofanya siku zote wakati wa vita.


Siku hiyo, ninasema mimi Yawe, nitamutia hofu kila farasi, na askari mupanda-farasi wake nitamufanya kuwa mwenda-wazimu. Farasi wa mataifa mengine nitawapofusha. Lakini kabila la Yuda nitalilinda.


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Wapiga upinde katika vita hawataweza kusimama na nguvu; wenye kuwa hodari kwa kukimbia mbio hawataweza kujiokoa, wala waaskari wapanda-farasi hawatayaokoa maisha yao.


kutoka kwenye makao yako, huko mbali kabisa upande wa kaskazini, ukuje pamoja na watu wengi wakiwa wote wamepanda farasi: jeshi kubwa na lenye nguvu.


Utawatafuta hao wanaopingana nawe, hautawaona tena; wale wanaofanya vita nawe, watakuwa wameangamia.


Yawe ataulinda mulima wa Sayuni, lakini watu wa Moabu watakanyagwakanyagwa ndani ya inchi yao kama nyasi katika shimo la mboleo.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Muungane, enyi watu wa mataifa, na kufezeheshwa! Musikilize, enyi inchi za mbali katika dunia! Mujiweke tayari na kufezeheshwa. Mujiweke tayari na kufezeheshwa.


Wewe ni muzuri kuliko wanadamu wote, maneno yako ni rehema tupu, Mungu amekubariki milele.


Mufalme hawezi kuokolewa kwa kuwa na kundi kubwa; wala shujaa hapati ushindi kwa nguvu zake kubwa.


Walitafuta musaada, lakini hakukukuwa wa kuwasaidia; walimulilia Yawe, lakini hakuwajibu.


Niliwatwanga, wakakuwa kama mavumbi, nikawaponda na kuwakanyaga kama matope katika barabara.


Halafu, dunia ikatetemeka na kutikisika, misingi ya mbinguni ikayumbayumba na kuruka, kwa maana Mungu alikuwa amekasirika.


Kijana mumoja kati ya watumishi akasema: “Nimemwona kijana mumoja wa Yese, wa muji wa Betelehemu. Kijana yule ana ujuzi wa kupiga kinubi. Yule kijana ni shujaa, hodari wa kupigana katika vita, ana hekima katika kusema na mwenye umbo zuri; Yawe yuko pamoja naye.”


Aliweza kuitwaa inchi hii yote kwa sababu Yawe, Mungu wa Israeli, aliwapigania Waisraeli.


Hakujakuwa siku kama hiyo hata kidogo wala haijapata kuonekana tena, siku ambayo Yawe amemwitikia mwanadamu kwa namna hiyo; maana Yawe mwenyewe aliwapigania Waisraeli.


“Mukienda kwa vita kupigana na waadui zenu, mukiona farasi, magari na jeshi kubwa zaidi kuliko lenu musiwaogope. Maana Yawe, Mungu wenu, aliyewatoa Misri, atakuwa nanyi.


Kisha nikaona malaika mumoja amesimama katika jua. Alikuwa akilalamikia ndege wote waliokuwa wakiruka juu katika anga akiwaambia: “Mukuje mukutane pamoja kwa karamu kubwa ya Mungu!


Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


Katika siku zile, Muyuda mumoja, jina lake Apolo, muzaliwa wa muji Alesanduria, alikuwa amefika katika muji Efeso. Alikuwa mutu mwenye uwezo katika masemi na mwenye kuelewa sana Maandiko.


Muwafundishe kutii maneno yote niliyowaagiza. Na mujue kwamba mimi ni pamoja nanyi siku zote hata mwisho wa dunia.”


Wewe ni mufalme wangu na Mungu wangu! Unawajalia ushindi wazao wa Yakobo.


Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.


Waisraeli watawashinda waadui zao na kuwaangamiza kabisa.


naye Yehu akawaambia: “Mumutupe chini!” Wakamutupa chini na damu yake ikasambaa juu ya ukuta na kwenye farasi. Yehu akapitisha farasi na gari lake juu ya maiti yake


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Swiv nou:

Piblisite


Piblisite